Balozi Faruk Kaymakci ahudhuria mkutano wa Kamati ya Pamoja ya Bunge la Turkiye na EU mjini Brussels, Ubelgiji tarehe 04 Desemba 2023. / Picha: AA

Umoja wa Ulaya unapaswa kuchukulia Uturuki kama nchi mgombea sawa, alisema balozi wa Uturuki katika umoja huo.

Katika mkutano wa maandalizi mjini Brussels siku ya Jumatatu kwa ajili ya mkutano wa 80 wa Kamati ya Pamoja ya Bunge la Uturuki na EU, uliopangwa kufanyika Desemba 19-20 katika mji mkuu wa Uturuki Ankara, Faruk Kaymakci alitoa maoni yake kuhusu ripoti mpya kuhusu uhusiano wa kisiasa, kiuchumi na kibiashara wa Uturuki na Umoja wa Ulaya, iliyowasilishwa wiki iliyopita na mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Josep Borrell na Kamishna wa Ulaya Oliver Varhelyi.

Ripoti hiyo ina hatua muhimu, lakini hazitoi nafasi ya kutosha kwa uhusiano wa Uturuki na Umoja wa Ulaya kukua katika maeneo muhimu, kulingana na Kaymakci.

Alisisitiza umuhimu wa kuichukulia Uturuki kama nchi mgombea sawa, akiongeza kuwa kusiwe na masharti ya kuanza mazungumzo ya kusasisha mkataba wa Umoja wa Forodha wa 1995.

Kaymakci pia alidokeza haja ya kuwezesha utoaji wa visa kwa raia wa Uturuki hadi makubaliano ya kuondoa viza utakapotolewa, kama ilivyoahidiwa chini ya mkataba wa 2016 kuhusu wahamiaji.

Ushirikiano wa kina katika mapambano dhidi ya ugaidi pia utaimarisha uaminifu kati ya pande hizo mbili, alisema, akiongeza kuwa miradi ya pamoja inapaswa kutekelezwa kwa wakimbizi wa Syria kurejea nyumbani kwa njia salama, ya hiari, ya heshima, hatua iliyotazamwa kwa muda mrefu na Uturuki, ambayo ni mwenyeji kwa zaidi ya wakimbizi milioni 3.6 wa Syria.

Kaymakci pia aliashiria jukumu muhimu la Uturuki katika vita vya Ukraine vilivyoanzishwa na Urusi na kutatua maswala ya Mashariki ya Kati.

Ukweli kwamba uhusiano wa NATO na EU hauko katika kiwango kinachotarajiwa kutokana na suala la Cyprus ambalo linadhoofisha uzuiaji wa Ulaya, moja ya sababu za vita vilivyoanzishwa na Urusi nchini Ukraine, alisema.

Taasisi kama vile Bunge la Umoja wa Ulaya haipaswi kutoa msingi mzuri wa kusaidia vikundi vya kigaidi, na ukosefu wa hatua dhidi ya ugaidi ndani ya EU husababisha ukosefu wa uaminifu katika uhusiano, Kaymakci pia alisema.

Uturuki, mgombea rasmi wa kujiunga na Umoja huo, iliomba uanachama wa Umoja wa Ulaya mwaka 1987, na mazungumzo ya kujiunga nayo yalianza mwaka wa 2005.

Tanga wakati huo, mazungumzo yamekwama kutokana na vizuizi vya kisiasa vya baadhi ya wanachama wa EU kwa sababu zisizohusiana na kufaa kwake kwa uanachama, kulingana na Ankara.

TRT World