"Ujumbe wangu kwa jumuiya ya kimataifa, ambao wanatuona wenyewe, ni kwamba sisi ni waandishi wa habari tumevaa vesti za kukinga silara. Kwa hivyo, kwa nini unatuona tumevaa helmeti? Kwa nini? Kwa sababu bado wanatulenga," mpigapicha wa TRT Arabi Sami Shehadeh alisema kufuatia shambulio hilo. . / Picha: AA

Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kufanyika uchunguzi wa uwazi na wa kuaminika kuhusu shambulio jipya la Israel kwenye kambi ya wakimbizi ya Nuseirat huko Gaza ya Palestina, ambalo lilijeruhi waandishi wa habari kadhaa wakiwemo wale wa idhaa ya TRT Arabi.

Shirika hilo limesisitiza kuwa mashambulizi ya Israel dhidi ya kundi la waandishi wa habari yanadhihirisha wazi hatari zinazowakabili waandishi wa habari huko Gaza.

Siku ya Ijumaa mchana, jeshi la Israel lililenga kwa makusudi kundi la waandishi wa habari waliokuwa wakiripoti kutoka kambi ya wakimbizi ya Nuseirat katikati mwa Gaza kwa moto wa tanki.

Mpigapicha wa TRT Sami Shehadeh, sehemu ya wafanyakazi wanaoripoti kutoka kambi ya wakimbizi ya Nuseirat katikati mwa Gaza, alijeruhiwa vibaya na madaktari waliishia kuukata mguu wake wa kulia.

Shehadeh, kufuatia shambulio hilo, alisema bado ataendelea kuwa sauti ya Gaza.

'Jimbo la kigaidi'

"Tunalaani shambulizi hili baya. Huu ni ugaidi. Ugaidi huu lazima ukomeshwe na ulimwengu wa Magharibi unapaswa kupinga ukatili huu haraka iwezekanavyo," Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Uturuki Fahrettin Altun alisema kufuatia tukio hilo.

"Hata iweje, tutaendelea kuueleza ulimwengu kuhusu ukatili wa Israel dhidi ya raia," aliapa akisisitiza kuwa Israel ni "taifa la kigaidi" ambalo linalenga waandishi wa habari kimakusudi ili kuficha ukatili wake na kuvuruga mtiririko wa habari.

Hii si mara ya kwanza kwa jeshi la Israel kuwalenga waandishi wa habari huko Gaza wakati wa vita vyake vinavyoendelea kwa zaidi ya nusu mwaka.

Kwa mujibu wa Ofisi ya Vyombo vya Habari vya Gaza, waandishi wa habari wasiopungua 140 wamepoteza maisha katika mashambulizi ya Israel katika eneo lililozingirwa, sasa ikiwa ni siku ya 189.

Mmoja wao alikuwa Montaser Al Sawaf, mpigapicha wa kujitegemea wa Anadolu, ambaye aliuawa katika mashambulizi ya anga ya Israel tarehe 1 Desemba kufuatia utulivu wa wiki moja wa kibinadamu kati ya Israel na kundi la muqawama la Palestina Hamas.

Mashambulizi hayo makali ya Israel yamesababisha vifo vya Wapalestina 33,545 na kuwajeruhi wengine 76,094 kwa jumla.

TRT World