Erdogan alisisitiza nia ya Uturuki kuchukua jukumu la mwezeshaji katika kukuza juhudi za mazungumzo na upatanisho, haswa katika muktadha wa hali inayoendelea nchini Ukraine. /Picha: Kumbukumbu ya AA

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na rais wa Urusi Vladimir Putin.

Wakati wa mazungumzo siku ya Jumatatu, alitoa pongezi kwa ushindi wa hivi majuzi wa Putin na kusisitiza dhamira ya Uturuki ya kukuza uhusiano mzuri kati ya nchi hizo mbili.

Rais Erdogan alielezea imani yake kwamba mwelekeo mzuri wa uhusiano wa Uturuki na Urusi utaendelea kuimarika katika kipindi kipya.

Pia alisisitiza nia ya Uturuki kuchukua jukumu la mwezeshaji katika kukuza juhudi za mazungumzo na upatanisho, haswa katika muktadha wa hali inayoendelea nchini Ukraine.

Jukumu la upatanishi la Uturuki katika vita vya Ukraine na Urusi

Uturuki, ambayo inmasifiwa kimataifa kwa nafasi yake ya kipekee ya mpatanishi kati ya Ukraine na Urusi, mara kwa mara ametoa wito kwa Kiev na Moscow kusitisha mapigano kupitia mazungumzo.

Juhudi za amani za Uturuki zilizaa matunda na matokeo muhimu, kama vile makubaliano ya kihistoria ya nafaka mnamo Julai 2022, na kubadilishana wafungwa wa vita kati ya Urusi na Ukraine. Moscow haikuongeza mkataba huo baada ya Julai 2023 ikitoa vizuizi kwa usafirishaji wa nafaka wa Urusi.

Uturuki iliandaa mkutano wa kwanza kati ya mawaziri wa mambo ya nje wa Urusi na Ukraine katika mji wa Mediterania wa Antalya mnamo Machi 2022.

TRT World