Mnamo Julai 17, Urusi ilisitisha ushiriki wake katika mkataba wa nafaka wa Bahari Nyeusi ili kuanza tena mauzo ya nafaka kutoka bandari tatu za Bahari Nyeusi za Ukraini ambazo zilisitishwa baada ya vita vya Ukraine kuanza Februari 2022. / Picha: AA Archive

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amewasili katika mji wa pwani wa Urusi wa Sochi kukutana na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin.

Katika ziara yake ya kikazi ya siku ya Jumatatu, Erdogan atajadili masuala ya sasa ya kikanda na kimataifa, pamoja na uhusiano wa Uturuki na Urusi na Putin.

Kufufua mkataba wa kihistoria wa nafaka wa Bahari Nyeusi ambao ulisaidia kupunguza mzozo wa chakula duniani pia itakuwa ajenda kati ya viongozi, ambao watafanya mkutano wa pamoja na wanahabari baadae.

Baada ya Urusi kusitisha ushiriki wake katika mkataba wa mauzo ya nafaka wa Ukraine, uliosimamiwa na Uturuki na Umoja wa Mataifa, UN, Ankara inaendelea na juhudi zake za kurejesha makubaliano hayo.

Moscow imelalamika kwamba nchi za Magharibi hazijatimiza wajibu wake kuhusu mauzo ya nafaka ya Urusi yenyewe, na kwamba nafaka ya Ukraine haitoshi ilikuwa ikienda kwa nchi zinazohitaji. Inasema vikwazo vya malipo, vifaa, na bima vimekuwa kikwazo kwa usafirishaji wake.

Akithibitisha umuhimu wa kutimiza matakwa ya Urusi ya kuuza nje nafaka na mbolea yake, Uturuki inasema hakuna mbadala wa mpango huo.

Ankara imekuwa ikifanya juhudi kubwa za kidiplomasia kwa ajili ya kurejesha mkataba wa Julai 2022 na pia imetoa wito kwa Kiev na Moscow kumaliza vita kwa njia ya mazungumzo.

Mnamo Julai, Erdogan pia alikutana na rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy huko Istanbul ili kujadili masuala hayo.

TRT World