Shughuli za uokoaji zimeanza, Wizara ya Ulinzi imesema / Picha: AA

Marubani wawili wamekufa baada ya ndege ya mafunzo kuanguka huko Kayseri, Wizara ya Ulinzi ya Uturuki imesema.

Imeongeza ya kuwa juhudi za utafutaji na uokoaji zimeanza.

Baada ya ripoti za ajali ya ndege ya mafunzo, timu za Utafutaji na uokoaji, na wazima moto zilitumwa katika kitongoji cha Hasan Arpa katika wilaya ya Kocasinan ya Kayseri.

TRT World