Fidan: "Nawaomba nyote muache vita hivi na uchokozi wa Israel." / Picha: AA

Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Hakan Fidan ameonya dhidi ya mashambulizi ya waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu huko Palestina na Lebanon.

"Kutokana na uvamizi wa Israel usio na mipaka, unaolenga Lebanon, sasa tuko katika hali isiyojulikana," Fidan alisema katika mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya Mashariki ya Kati. "Mashambulizi makali ya mabomu yanaendelea bila kusitishwa, bila kutofautisha raia na walengwa wa kijeshi."

Kauli yake hiyo imekuja baada ya jeshi la Israel kufanya mashambulizi makali ya anga na ambayo hayajawahi kutokea katika eneo la kitongoji cha kusini mwa Beirut na kudai kushambulia makao makuu ya kundi la Lebanon la Hezbollah.

Baraza la Usalama linapaswa kuchukua "kazi yake kwa umuhimu," alisisitiza. "Nawaomba nyote muache vita hivi na uchokozi wa Israel."

"Leo, tunakabiliwa msumeno mbaya, hatua kali y amageuzi, mpangilio wetu wa msingi wa sheria unaothaminiwa uko katika hali mbaya.

"Mmomonyoko huu unazidi kutoweza kutenduliwa kila kukicha. Hekima inadai kusimamisha vita hivi vya kinyama huko Gaza kabla ya kuenea hadi Ukingo wa Magharibi, Lebanon na kwingineko," alisema Fidan.

Mpango wa kusitisha mapigano mara moja

Waziri huyo alikosoa watendaji wa kimataifa ambao "hawaonyeshi mawazo yoyote kuchukua hatua madhubuti" ingawa wana uwezo wa kubadilisha "matendo haya ya kutisha."

Fidan alidai makubaliano ya mara moja ya kusitisha mapigano huko Gaza na kusema Netanyahu "amekwepa mara kwa mara makubaliano kama hayo kutekelezwa."

Fidan alisema Netanyahu ataendeleza "vitendo vyake vya mauaji ya halaiki" hadi jumuiya ya kimataifa, haswa Baraza la Usalama, litakapoweka "shinikizo la kweli" kwa Israeli kuacha mauaji, na kusisitiza kuwa Baraza hilo "kwa masikitiko makubwa" limeshindwa kuhakikisha kuwa Israel inatekeleza maazimio yake.

Amani ya "pekee" itahakikisha usalama wa Israeli na kwamba amani itakuja "tu" kupitia suluhisho la serikali mbili kati ya Israeli na Palestina.

"Maslahi ya kisiasa au ya kibinafsi ya Netanyahu na washirika wake wa kimsingi haipaswi kuhatarisha utulivu wa kikanda na utaratibu wa kimataifa," aliongeza.

Uturuki inaunga mkono kwa dhati suluhu la mataifa mawili katika mzozo wa Israel na Palestina, ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa taifa huru la Palestina lenye msingi wa mipaka ya 1967, Jerusalem Mashariki ikiwa mji mkuu wake.

"Tushirikiane sote kwa ajili ya amani ya haki na ya kudumu. Huu ni wito wetu kwa Baraza la Usalama," aliongeza Fidan.

TRT World