Mtu huyo anayezuiliwa na shirika la kijasusi la Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Iran katika mji wa Parsabad katika mkoa wa Ardabil nchini Iran. / Picha: Reuters Archive

Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Irani lilitangaza kukamatwa kwa mmoja wa wasimamizi wa Kundi la Turan, ambalo Tehran inadai kuwa na malengo ya kupanua ushawishi wa Kituruki.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Tasnim, mtu anayedaiwa kujihusisha na utaifa wa kikabila huku akiwasiliana na watu nje ya nchi, alizuiliwa na shirika la kijasusi la Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Iran katika mji wa Parsabad katika mkoa wa Ardabil nchini Iran.

Waturuki nchini Iran

Sehemu kubwa ya wakazi wa Iran wanatoka katika makabila yenye asili ya Kituruki.

Baadhi ya makundi haya yametoa madai ya ubaguzi dhidi ya Waturuki na kulalamikia majaribio ya kuwaingiza katika utamaduni wa Kiajemi.

Serikali ya Irani linafuatilia makabila haya, ambayo yanachukuliwa kuwa yanapinga serikali na yanaitwa vikundi vya Pan-Turkist.

TRT World