Erdogan, Aby Ahmed wajadili mvutano wa kikanda katika mazungumzo ya simu

Erdogan, Aby Ahmed wajadili mvutano wa kikanda katika mazungumzo ya simu

Juhudi za upatanishi za Uturuki kutatua mvutano kati ya Somalia na Ethiopia zinaendelea.
  Erdogan aliitaka Ethiopia kuunga mkono hoja ya Palestina dhidi ya mauaji ya kimbari ya Israel. / Picha: Jalada la AA  

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amezungumza na Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed katika mazungumzo ya simu kuhusu uhusiano wa nchi mbili, mivutano ya kikanda na maendeleo ya kimataifa.

Viongozi hao wawili walijadili maeneo muhimu ya ushirikiano kati ya Uturuki na Ethiopia, wakipongeza kuimarika kwa uhusiano kati ya mataifa hayo mawili, Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki ilisema Ijumaa katika taarifa yake kwenye X.

Wakati wa simu hiyo, Erdogan aliangazia juhudi zinazoendelea za Uturuki kupatanisha mvutano kati ya Somalia na Ethiopia.

Aidha alibainisha kuwa hatua zitakazochukuliwa na Ethiopia kuondoa wasiwasi wa Somalia kuhusu umoja wake, mamlaka yake na uadilifu wa eneo zitasaidia mchakato huo.

Duru ya awali ya mazungumzo ya moja kwa moja kati ya mawaziri wa mambo ya nje wa Ethiopia na Somalia ilifanyika katika mji mkuu wa Uturuki Ankara mapema Julai. Ilisababisha vyama hivyo kukubaliana kukutana tena kwa duru ya pili mnamo Septemba 2.

Mbali na masuala ya kieneo, Erdogan amelaani vita visivyokoma vya Israel dhidi ya Gaza ya Palestina na kusisitiza kuwa Tel Aviv inadumisha mauaji ya halaiki katika eneo hilo linalozingirwa.

Rais alieleza kuwa uungaji mkono wa Ethiopia kwa kadhia ya Palestina kwa kupendelea dhamiri ya ubinadamu utachangia katika juhudi za jumuiya ya kimataifa za kuleta amani ya kudumu.

TRT World