Kulingana na wachambuzi wa siasa, uhuisiano kati ya Saudi na UAE ni mchanganyiko wa uhusiano mzuri, mvutano, na uhalisia. /Picha: AFP    

Na

Giorgio Cafiero

Wataalamu wa Mashariki ya Kati wana maoni mbalimbali kuhusu uhusiano wa Mwana Mfalme wa Saudi na Waziri Mkuu Mohammed bin Salman (MBS) na Rais wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) Mohammed bin Zayed (MBZ).

Baadhi ya wachambuzi wanashikilia kuwa mzozo unaodaiwa kuwa kati ya viongozi hao wawili wa Kiarabu ni mkubwa kiasi kwamba hivi karibuni nchi zao zitakoma kuwa washirika, huku wengine wakiashiria mkutano kati ya viongozi hao wawili uliofanyika mwezi uliopita mashariki mwa Saudi Arabia kuwa ni ishara kwamba hakuna mivutano mikubwa.

Huenda ukweli ukawa uko katikati.

Wakati uhusiano wa kikanda kati ya mataifa hayo mawili ni ngumu kukatika - kama walivyofanya na Qatar mwaka 2017 - Riyadh na Abu Dhabi zina vipaumbele tofauti, ikiwemo misimamo, na maslahi ambayo yamezua matatizo. Kuanzia suala la kurekebisha uhusiano na Israeli hadi mizozo fulani barani Afrika kama vile vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Sudan, maslahi ya Saudia na Imarati hayawiani, kwa hivyo kwa kawaida mvuatno fulani upo katika masuala ya nchi mbili.

Pia kuna ongezeko kubwa la ushindani wa kiuchumi kati ya mataifa haya mawili ya Baraza la Ushirikiano la Ghuba (GCC) huku zote zikifuatilia mipango yao ya maendeleo na ya kiuchumi tofauti.

Mahusiano mazuri

"Akiwa mkubwa kati ya viongozi hawa wawili, [MBZ] anatarajia kupewa heshima, ndiyo maana kutoelewana mara kwa mara hujitokeza," alielezea Joseph A. Kechichian, mwandamizi katika Kituo cha King Faisal huko Riyadh, katika mahojiano na TRT World.

MBZ ni kiongozi wa kikanda ambaye anapenda kuweka mwelekeo na kutekeleza ushawishi wake kwenye jukwaa la kimataifa.

Maswali kuhusu jinsi uhusiano wake na MBS utakavyokuwa, MBS ni kiongozi mchanga na mwenye kujiamini kutoka Saudia, akinyoosha misuli yake mwenyewe kwani mtawala mkuu wa nchi kubwa ya Kiarabu, yamekuwa yakichochea midahalo ya kuvutia.

"Kwa makadirio yangu, njia bora ya kuelezea uhusiano kati ya nchi hizo mbili kwa wakati huu ni kwamba ni mchanganyiko wa uhusiano mzuri, mvutano, na uhalisia," Aziz Alghashian, mwanachuo katika Chuo Kikuu cha Lancaster, aliiambia TRT World.

Mvutano kati ya MBS na MBZ hauna uhasimu mkali, kulingana na Hussein Ibish, mwanachuoni mkuu katika Taasisi ya Arab Gulf States huko Washington. Badala yake, alizitaja kama sehemu ya "uhusiano unaoweza kudhibitiwa" ambao ni mzuri zaidi kuliko uhasiano wa udanganyifu kati ya nchi hizo mbili uliochochewa baada ya machafuko ya nchi za Kiarabu mwaka 2011, yakiwa pamoja na migogoro ya silaha yalikuwa yaliosababisha ukosefu wa utulivu katika eneo la Mashariki ya Kati.

"Ijapokua nchi hizo mbili bado zinapimana nguvu za kiuchumi na kisiasa na hata kijeshi," Ibish aliongeza.

Mnamo 2021, mamlaka nchini Riyadh ilitoa amri kwa kampuni za kigeni zilizo na uwepo nchini Saudi Arabia kuwa na makao makuu yao nchini humo kuanzia mwaka wa 2024.

Ingawa mamlaka ya Saudi Arabia iliashiria jinsi hii ilikuwa sehemu ya muda mrefu wa maendeleo ya nchi, hatua hii inaonekana kuwa ni changamoto kwa nafasi ya UAE katika eneo hilo, ambapo makampuni mengi ya kigeni yanayofanya kazi katika Ghuba za Kiarabi zina makau makuu yake.

Yemen, chanzo cha ugomvi

Kulinagana na wachambuzi wa usalama wa Mashirika ya Kati, Yemen ndio chanzo kikubwa cha mzozo kati ya Saudi Arabia na UAE.

Kuanzia Machi 2015, Riyadh na Abu Dhabi kwa pamoja ziliongoza muungano wa kijeshi wa Waarabu uliolenga kupunguza makali ya Houthi ya 2014/15.

Lakini miaka kadhaa katika kampeni hiyo, uongozi wa UAE ulitambua jinsi kampeni hio ilivyokuwa hatari na hatimaye kubadili mkondo.

Mnamo mwaka wa 2019, UAE iliondoa rasmi vikosi vyake kutoka Yemen na kuanza kulenga kuathiri mazingira ya kusini mwa Yemen kupitia watendaji wengine wasio wa serikali.

Hii ilihusisha UAE kuunga mkono makundi mbalimbali ya Yemen kama vile Baraza la Mpito la Kusini (STC), huku ikiacha Saudi Arabia kupigana na Houthis kaskazini mwa Yemen.

"Ukweli ni kwamba UAE [na] Saudi Arabia ziliingia Yemen na ajenda tofauti. Baada ya muda, hilo lilikuja kuwa dhahiri zaidi kuliko ilivyokuwa [mwanzoni],” alisema Ibish.

Hakuna ubishi kwamba mizozo kama hiyo ya kimaslahi kati ya Saudi Arabia na UAE dhidi ya Yemen imeunda mienendo katika msingi ambayo inahudumia maslahi ya Houthi na yale ya Iran.

Kukosekana kwa maelewano kati ya Riyadh na Abu Dhabi kumekuwa sababu kubwa inayochangia udhaifu na kutofanya kazi kwa Baraza la Uongozi wa Rais (PLC), ambalo ni barazi linaloongoza serikali ya Yemen linalotambulika kimataifa, linapokuja suala la kushughulika na Wahouthi.

STC inayofadhiliwa na UAE inapinga viongozi wanaoungwa mkono na Saudi Arabia nchini Yemen ambao wanatafuta kujitenga kwa Kaskazini-Kusini mwa Yemen. Kama Kechichian alivyoeleza, uungaji mkono wa Abu Dhabi kwa STC, ambayo inataka kuanzishwa upya kwa taifa huru la Yemen Kusini ambalo lilikuwepo hapo awali kutoka 1967-90, umesababisha "tofauti kubwa" kati ya sera za kigeni za Saudi na UAE huko Yemen.

Washirika hao wawili wa GCC wanaunga mkono makundi tofauti ya Yemeni ambayo, kwa madhumuni yote ya kiutendaji, yanaendeleza mgawanyiko, anaelezea Kechichian.

Akiongeza, Riyadh na Abu Dhabi hazionekani kuwa tayari kuweka kando tofauti zao na kuunga mkono uongozi mmoja ambao unaweza kuwashinda Wahouthi, kudumisha umoja wa Yemen, na kuwekeza katika ujenzi wake upya.

Veena Ali-Khan, mtafiti wa Yemen na Ghuba ya Uajemi, aliiambia TRT World, "Bado kuna uvumi kwamba [UAE] inashinikiza kuchukua udhibiti wa bandari ya Aden kupitia Dubai Ports World.

Muhimu zaidi, mgawanyiko mkubwa bado upo ndani ya vikosi vya kupambana na Houthi, na uhasama unaoongezeka kati ya vikosi vya STC na Amalika, ambavyo vinadaiwa kuwa upande mmoja. Ili kuiweka wazi, ajenda zinazopingana na za Saudi Arabia na UAE nchini Yemen bado zinachangia kugawanyika kwa PLC.

Hata hivyo, hadi sasa Riyadh na Abu Dhabi zimeweza kudhibiti tofauti zao nchini Yemen, kutokana na kuchochea mgogoro wa pande zote katika masuala ya pande mbili, hata kama baadhi ya wafafanuzi wametumia miaka mingi kudokeza ya kwamba muungano wa Saudi-UAE unazidi kuzoroteka.

Hisa za Saudia huko Yemen Kusini

Uongozi wa Saudi utazingatia kubaki kwa hali ilivyo sasa au mabadiliko katika nchi ya Yemen iliyogawanyika.

Kuna sababu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na ukweli kwamba Riyadh haiamini kuwa inaweza kutoa ushawishi wa kutosha katika nchi huru ya kusini mwa Yemen ambayo inaweza kuibuka tena katika siku zijazo.

Hata hivyo, watunga sera huko Riyadh wanaweza kuachwa katika hali ambayo itawabidi kuruhusu kusini mwa Yemen kujitenga kwa utaratibu.

"Nadhani [maafisa wa Saudi] wangelazimika tu kukubali kuwa ni jambo la kawaida, lakini hawatalipenda. Sio kwa maslahi yao. Ikiwa wanaweza kufanya lolote kuhakikisha halifanyiki, watafanya,” Ibish alisema.

Wataalamu wengine wanakubali. "Wanasema, Yemen Kusini ikipata uhuru ingeleta changamoto kubwa kwa Riyadh ambayo pengine isingekaribisha vikosi vyovyote vya kujitenga kwenye eneo hilo la Ghuba, jambo ambalo GCC-inawezekana-haingependa kuona pia," Kechichian aliiambia TRT World.

Lakini iwapo mgawanyiko kama huo wa Yemen utatokea, kwa njia ya rasmi au nyingine, Riyadh inaweza kuchukua hatua kwa uangalifu ili kuepusha kuzidisha mivutano ambayo inaweza kurudisha nyuma maslahi ya usalama wa kijiografia ya Saudi Arabia.

"Natarajia wasomi wa Saudia watatathmini jinsi Yemen Kusini huru itakavyoathiri utulivu kwenye mpaka wa Saudi," alisema Alghashian.

"Kwa Saudi Arabia, imedhihirika kuwa iko tayari kuwa na uhalisia kuhusu nani inafanya uhusiano naye. Kwa kusema hivyo, sioni Wasaudi wamekaa tu na kuruhusu STC kutawala kusini. Kwa hivyo, kama taifa la Yemen Kusini litazinduliwa, hii itamaanisha kuwa Yemen zote mbili zitasimamiwa na kuwa mwendelezo wa ushindani wa Saudi-UAE kwa miaka ijayo," aliongeza.

Mienendo ya kikanda

Ushindani mkali na viwango vya juu vya mvutano kati ya mataifa ya GCC vimekuwepo kila wakati.

Hata hivyo, katika historia mivutano hii imeweza kutulia zaidi wakati wa mgogoro katika eneo hilo.

Hivi ndivyo hali ilivyo leo huku kukiwa na vita vya Israeli dhidi ya Gaza, ambavyo vimeenea hadi kwenye Bahari Nyekundu na huenda vinaweza kusababisha vita vikali nchini Lebanon.

Katika muktadha huu, kuna uwezekano MBS na MBZ, kama viongozi wa kivitendo, watapunguza na kudhibiti mivutano kati ya nchi zao kuhusiana na Yemen; kutengwa kwa, lakini amabayo haijatatuliwa.

Baada ya hatimaye kusitishwa kwa mapigano huko Gaza na ghasia katika Bahari Nyekundu, kusini mwa Lebanon, na kaskazini mwa Israeli kuwa chini ya udhibiti mkubwa, itakuwa muhimu kufuatilia jinsi mvutano wa Riyadh-Abu Dhabi kuhusu mustakabali wa Yemen unavyofanyika.

Giorgio Cafiero ni Mkurugenzi Mtendaji wa Uchanganuzi wa Nchi za Ghuba (@GulfStateAnalyt), akiwa na makao yake Washington, DC.

TRT Afrika