Migogoro ya mipaka kati ya Hezbollah na Israeli / Picha: Reuters

Na Mahjoob Zweiri

Siku ya Jumanne, Iran ilifanya shambulizi dhidi ua Israeli, lililolenga vifaa vyao vya kijeshi katika operesheni iliyopewa jina "True Promise 2."

Ikumbukwe kuwa, awamu ya kwanza ya "True Promise" ilitokea mwezi Aprili, baada ya Israeli kushambulia ubalozi wa Iran mjini Damascus.

Kwa mujibu wa Marekani, shambulio la wiki hii lilikuwa kubwa, mara mbili zaidi ya lile la Aprili, hasa baada ya Iran kutuma makombora 200 yenye nguvu katika miji mbalimbali na katika ngoma za jeshi la anga nchini Israeli.

Kufuatia shambulio hilo, Iran ilionya kwamba, iwapo Israeli itajibu mapigo, basi iwe tayari kushuhudia uharibifu mkubwa wa miondombinu yake. Kwa sasa, Iran imehalalisha shambulizi hilo, ikisisitiza kuwa Israeli imekuwa ikitishia usalama wake, siasa zake na utulivu wake kwa mwaka jana.

Malengo ya Netanyahu

Mauaji ya kiongozi wa Hezbollah Hassan Nasrallah na maofisa wengine wa kijeshi ambao walikuwa ni sehemu ya uongozi wa Iran inaonesha wazi kuwa Israeli ina nia ya kuharibu mtandao wa Iran huko Mashariki ya Kati.

'Iran imefanya makosa makubwa na watalipa kwa ajili ya hilo kosa,' Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu alisema.

Mbali na hayo, mashambulizi makali ya Israel dhidi ya vituo vya Hezbollah kusini mwa Lebanon na uvamizi wa hivi majuzi dhidi ya nchi hiyo yanatoa ujumbe wa wazi: baada ya kuiangamiza Gaza na kushindwa kufikia lengo lake la kuitokomeza Hamas, Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu ameamua kuendeleza vita kwa Hezbollah.

Kuanzishwa kwa Iran kunaonekana kufahamu vyema mkakati wa Netanyahu wa pande tatu. Kwa hivyo ni lazima ilishambulia Israeli kupinga mpango huu, ambao ulilenga kuunda upya Mashariki ya Kati, kama Netanyahu alivyodai baada ya mauaji ya Nasrallah.

Licha ya kwamba mashambulizi ya Jumanne yalilenga kambi za kijeshi, ujumbe wa Iran ulikuwa ni kwamba, iwapo hatua yoyote ya kukabiliana nayo itachukuliwa na serikali ya Israel, kutakuwa na majibu makali. Iran pia ilituma ujumbe wa wazi kwa washirika wa Israel, kwamba ikiwa Tel Aviv itapokea msaada wa aina yoyote wa kijeshi ili kuidhuru Iran, Tehran pia italipiza kisasi dhidi ya nchi hizo - ujumbe unaolekezwa kwa Marekani moja kwa moja.

Tishio la Iran

Swali kubwa kwa sasa ni; Israeli itajibu vipi? Kupata majibu, ni muhimu kukumbuka kuwa kwamba kwa zaidi ya miaka 20 sasa, Netanyahu ameichukulia Iran kama tishio kubwa kwa mikakati yake ya kisiasa na kiuchumi katika eneo la Mashariki ya Kati.

Iran pia ilituma ujumbe wa wazi kwa washirika wa Israel, kwamba ikiwa Tel Aviv itapokea msaada wa aina yoyote wa kijeshi ili kuidhuru Iran, Tehran pia italipiza kisasi dhidi ya nchi hizo - ujumbe unaolekezwa kwa Marekani moja kwa moja./Picha: Getty

Mtazamo huu umetokana Iran kukataa kuitambua Israeli, uamuzi wake wa kuunga mkono harakati za upinzani, na kutoa changamoto kwa uwezo wa kijeshi wa Israeli kwa kutengeneza miradi ya makombora.

Mzozo unaowezekana na Iran ulimchochea Netanyahu kujadili Mkataba wa Abraham mnamo 2020, ambao ulijumuisha kughushi makubaliano na Umoja wa Falme za Kiarabu na Bahrain. Zaidi ya hayo, Netanyahu alijaribu kutatiza matokeo ya mkutano wa amani wa Madrid wa 1991 na mchakato wa Oslo wa 1993.

Pia alijaribu kuvunja mradi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA). Na katika juhudi za kupunguza nafasi ya Iran katika Mashariki ya Kati, Netanyahu amekuwa akifanya kazi ya kukandamiza nguvu na ushawishi wa Hamas na Hezbollah huko Gaza na kusini mwa Lebanon.

Mkakati wa Israeli

Kwa vyovyote vile, Israeli inaweza kutumia shabaha mbili kuu nchini Iran ambazo zinaweza kuipa Tel Aviv uhalali na uungwaji mkono wa Marekani na nchi nyingine za Ulaya, na shabaha hizo ni vituo vya makombora vya balistiki vya Iran na vifaa vya nyuklia.

Takwimu za Bloomberg zinaonesha wazi kile kinachoendelea kati ya Israeli na Lebanon. Kwanza, licha ya mazungumzo yote ya tishio la roketi za Hezbollah kugonga Israeli, ni Israeli ambayo mara kwa mara inarusha makombora mengi zaidi kwenye mpaka.

Hali kama hii ikijitokeza, Iran itakuwa haina budi kujibu. Na kwa kuzingatia shambulio lake dhidi ya Israeli wiki hii, Tehran hakika imezingatia hali ya kulipiza kisasi na kuimarisha usalama kwa shabaha kama hizo.

Kama nyongeza, Netanyahu atawalenga watu na wanasiasa wenye uhusiano na Iran au labda Iran yenyewe. Hii itakuwa kama msaada wa kisaikolojia kwa umma wa Israeli, ambao utamrejeshea Netanyahu mtaji wake wa kisiasa.

Bila kujali mkakati wake, jibu la Israeli linaweza kufungua sura mpya ya mzozo katika Mashariki ya Kati. Marekani pia itajaribu kuzuia kuingilia moja kwa moja kabla ya uchaguzi wake, ambao utafanyika Novemba 5.

Kwa kuhitimisha, ingawa Israeli na Marekani zinadai kwamba shambulio la Iran lilishindwa wiki hii, mtazamo huo unatarajiwa kudhoofisha madai yoyote ya ushindi ambayo yanaweza kutolewa na Iran na washirika wake.

Shambulizi lenyewe limepinga mkakati wa Netanyahu wa kulenga Iran baada ya uvamizi wa ardhini kusini mwa Lebanon. Aina hii ya shambulio huenda likafungua eneo hilo kwa kutokuwa na uhakika zaidi wa siasa na usalama na mashambulizi mabaya ya duru na mashambulizi katika Mashariki ya Kati.

Mwandishi wa maoni haya ni Profesa wa siasa za Mashariki ya Kati na mtaalamu wa mambo ya Iran kutoka Chuo Kikuu cha Qatar.

TRT Afrika