Wakuu wa nchi na serikali wa IGAD watakutana nchini Uganda Januari 18, 2024. / Picha: TRT Afrika

Serikali inayoungwa mkono na jeshi la Sudan siku ya Jumamosi ilipuuza mwaliko wa mkutano wa kilele wa Afrika Mashariki na kukemea Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na kamanda wa vikosi hasimu vya kijeshi RSF.

Miezi tisa baada ya vita kuzuka kati ya jeshi la kawaida na Wanajeshi wa Msaada wa Haraka (RSF), jeshi limekuwa likipoteza eneo lake wakati kiongozi wa kijeshi Mohamed Hamdan Dagalo amekuwa akizuru miji mikuu ya Afrika ili kuongeza hadhi yake ya kidiplomasia.

Likikataa mwaliko wa kambi ya Afrika mashariki IGAD katika mkutano wa kilele nchini Uganda Januari 18 utakaohudhuriwa pia na Dagalo, baraza la mpito la mamlaka ya Sudan linaloongozwa na mkuu wa majeshi Abdel Fattah al-Burhan, lilisisitiza: "Matukio ya Sudan ni suala la ndani. "

Umoja huo umejaribu mara kwa mara kuwa mpatanishi kati ya majenerali wanaopigana wa Sudan, lakini juhudi zake zimezuiliwa na serikali ya Burhan.

"Kimya kama kaburi"

Kwa upande wake, Dagalo, ambaye ametoka katika ziara ya kutembelea miji mikuu sita ya Afrika, alisema kwenye X, ambayo zamani ilikuwa Twitter, kwamba amekubali mwaliko kutoka kwa IGAD na atahudhuria mkutano huo nchini Uganda.

Wizara ya mambo ya nje ya Sudan ilisema kualika Dagalo ni "ukiukwaji mkubwa" na "kunaharibu uaminifu wa IGAD" kama taasisi.

"Siyo tu kwamba IGAD imekuwa kimya kama kaburi juu ya ukatili wa wanamgambo, pia imetaka kuwapa wanamgambo uhalali kwa kuwaalika kwenye mkutano uliohudhuriwa na wakuu wa nchi wanachama na serikali," ilidai.

Burhan amejibu kwa hasira kuhusu kuongezeka kwa hadhi ya kidiplomasia ya Dagalo, akiwashutumu viongozi wa Afrika waliomkaribisha katika ziara yake ya hivi majuzi ya kushiriki katika ukatili dhidi ya raia wa Sudan.

Zaidi ya 13,000 waliuawa

Vita hivyo vimeua zaidi ya watu 13,000, kulingana na makadirio ya kihafidhina ya mradi wa Armed Conflict Location & Event Data.

Raia wapatao milioni 7.5 wamekimbia mapigano, kulingana na takwimu za Umoja wa Mataifa.

Pande zote mbili zimekuwa zikishutumiwa kwa uhalifu wa kivita, ikiwa ni pamoja na uvamizi wa makombora kiholela katika maeneo ya makazi, mateso na kuwekwa kizuizini kiholela kwa raia.

'Ukiukaji wa kutisha'

Sadiq alisema alimfahamisha Lamamra kwamba simu ya mkuu wa Umoja wa Mataifa siku ya Alhamisi ilitumika "kuhalalisha" Dagalo, "kiongozi wa vuguvugu ambalo limefanya ukiukwaji wa kutisha ambao umelaaniwa na baadhi ya taasisi za Umoja wa Mataifa pamoja na wengi wa jumuiya ya kimataifa."

Lamamra aliteuliwa kuwa mjumbe wa Guterres kwa Sudan, baada ya kusitishwa kwa ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo mwezi uliopita kwa ombi la serikali ya Burhan.

TRT Afrika