Mwendesha mashtaka wa serikali ya Nigeria alisema katika hati ya mashtaka hatua ya waandamanaji wakati wa maandamano ya Agosti 1-10 ni sawa na uhaini. / Picha: Reuters

Nigeria imewafungulia mashtaka watu kumi walioshiriki maandamano ya kuipinga serikali yaliyofanyika nchi nzima mwezi uliopita kwa kosa la uhaini.

Waandamanaji hao kumi walishtakiwa mbele ya Mahakama Kuu ya Shirikisho huko Abuja, mji mkuu wa nchi hiyo, na serikali muda wa mwezi mmoja tu baada ya kukamatwa na polisi.

Mwendesha mashtaka wa serikali alisema katika hati ya mashtaka hatua ya waandamanaji wakati wa maandamano ya Agosti 1-10 ni sawa na uhaini na uchochezi wa jeshi kupindua serikali ya kidemokrasia, vyombo vya habari vya ndani viliripoti.

Mawakili wa waandamanaji hao waliiomba mahakama kuwapatia washtakiwa hao (waandamanaji) dhamana kabla ya kufunguliwa kwa kesi hiyo Septemba 11.

Siku kumi za maandamano nchi nzima

Hakimu, hata hivyo, aliamuru waandamanaji hao wazuiliwe katika gereza moja katika mji mkuu wa taifa hilo wakisubiri kuamuliwa kwa ombi la dhamana lililopangwa kufanyika Septemba 11.

Maelfu ya vijana, wanaharakati na wanasheria walifanya maandamano ya siku kumi nchini kote kupinga gharama kubwa ya maisha, matatizo ya kiuchumi na ukosefu wa usalama katika taifa hilo la Afrika Magharibi licha ya rufaa kadhaa za Rais Bola Tinubu.

Maandamano hayo baadaye yalibadilika na kuwa vurugu na uharibifu wa majengo ya umma.

Takriban waandamanaji 2,000 walikamatwa wakati na baada ya maandamano hayo, kwa mujibu wa polisi.

TRT Afrika