Hakuna video yoyote kati ya hizi zilizoenezwa inahusiana na vita ya sudan

Hakuna video yoyote kati ya hizi zilizoenezwa inahusiana na vita ya sudan

Taarifa potofu zimetumika sana katika kuchochea vita wakati wa mzozo wa madaraka Sudan
Kueneza migogoro na hofu wakati wa vita Sudan unaendelew / Photo: AP

Na Kevin Philips Momanyi

Mitandao ya kijamii ni kitovu cha habari potofu na upotoshaji, haswa katika maeneo yenye vita. Hivi majuzi, Twitter ilitumika kama chanzo kikuu baada ya Elon Musk, mmiliki mpya wa kampuni hiyo, kuanza kuondoa alama za uthibitishaji za bluu kutoka kwa watumiaji ambao hawajajisajili kupata huduma hiyo.

Watumiaji hawa walijumuisha wanahabari, wasomi, na baadhi ya watu mashuhuri. .

Kueneza migogoro na hofu wakati wa vita kunaweza kuendelezwa kwa kushindwa kudhibiti taarifa za uwongo au za kupotosha kwenye mitandao ya kijamii

Taarifa potofu zimetumika sana katika kuchochea vita wakati wa mzozo wa madaraka kati ya Abdel Fattah al-Burhan na Mohamed Dagalo, wapinzani wawili katika jeshi la Sudan katika vita ambavyo vimepelekea takriban watu 300 kuuwawa.

Licha ya maombi ya kusitisha mapigano, mapigano bado yanaendelea, na watumizi wa mitandao kwa ujumla wamekua wakisambaza habari za uwongo.

Hizi ni baadhi ya habari za uwongo maarufu ambazo zimesambaa wakati wa mzozo wa Sudan.

Tweet ya video inayoonyesha jeshi la Sudan likiharibu makao makuu ya kundi pinzani la wanamgambo wa RSF ni uongo. Video asili ilitiwa kwenye YouTube nchini Yemen miaka miwili iliyopita na kituo kwa jina Ana_Al_Fahad. Maandishi ya waridi yenye maandishi "@Ana_Al_Fahad" yanaweza kuonekana chini,kulia mwa video.

Jeshi la Sudan lkuharibu makao makuu ya kundi pinzani la wanamgambo wa RSF ni uongo.

Tweet ya video inayodai kuwa simba alitoroka mbuga ya wanyama na kuonekana akirandaranda mitaani huko Khartoum, Sudan, wakati wa mzozo unaoendelea ni ya kupotosha.Video asili ilinaswa kutoka ndani ya gari katika wilaya ya Benghazi,Benina nchini Libya.

Simba atoroka mbuga ya wanyama na kuonekana akirandaranda mitaani huko Khartoum, Sudan

Picha za uwongo pia zimesambazwa ambazo zinadai kuonyesha vikosi vya Sudan vikiondoka Ethiopia mnamo Aprili 2023. Utafutaji wa picha za kinyume kwenye Google unaonyesha kuwa picha hizo hazihusiani na tukio hilo linalodaiwa.

Tweet hii yenye picha zinazodaiwa kuwa wanajeshi wa Sudan wakiondoka Ethiopia kutokana na mzozo wa nchi yao mwezi Aprili 2023 ni UONGO.

Picha zinazodaiwa kuwa wanajeshi wa Sudan wakiondoka Ethiopia kutokana na mzozo wa nchi yao mwezi Aprili 2023 

Picha hizo zilichapishwa kwa mara ya kwanza na tovuti ya Getty Images hapa tarehe 3 Mei 2015, na tovuti ya Sudan Tribune hapa tarehe 19 Machi 2022, hapa tarehe 5 Machi 2023 na hapa tarehe 6 Agosti 2022 mtawalia.

Video nyingine inayozunguka kwenye Twitter ikidai kuwa wanajeshi nchini Sudan wameanza kuua raia ni uongo. Eneo la Gambela la Ethiopia, si Sudan, ndipo video ilichukuliwa mwaka wa 2022. Filamu hii ina ushahidi wote tunaohitaji ili kuunga mkono hitimisho letu.

Mmoja wa wanajeshi waliopo kwenye video hiyo anaonekana akiwa amebeba chupa ya maji ambayo imetengenezwa na kampuni ya "Mogle Bottled Water Manufacturing", ambayo inazalisha maji ya chupa kwa jina la "One Water" yenye makazi yake Sebeta, kusini magharibi mwa Addis Ababa, Ethiopia.

Ripoti kuwa wanajeshi nchini Sudan wameanza kuwaua raia si kweli

Bendera ya Ethiopia ya eneo la Gambella inaonekana upande wa juu kushoto wa shati la askari huyo anapoingia kwenye video. Machafuko nchini Somalia hayana uhusiano wowote na video hiyo.

Madai yaliyotolewa kwenye video kwamba helikopta za kijeshi zinaruka juu ya Sudan ni uongo. Mnamo 2022, video ilichapishwa kwa mara ya kwanza katika siku ya kwanza ya kumbukumbu ya miaka 68 ya jeshi la Sudan katika gwaride la kijeshi. Video hii haihusiani kwa lolote na machafuko nchini Sudan.

Helikopta za kijeshi zinashika doria juu ya Sudan

Haya hayatakuwa matukio ya kwanza ya habari za uwongo kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii, wala hayatakuwa ya mwisho. Ni muhimu kukumbatia ukaguzi wa ukweli, hasa wakati huu wa mgogoro nchini Sudan, kabla ya kushiriki chochote ili kuhimiza watumiaji wa mitandao ya kijamii kueneza ukweli badala ya taarifa ghushi.

TRT Afrika