'Enzi mpya': Ramaphosa wa Afrika Kusini aapishwa kwa muhula wa pili

'Enzi mpya': Ramaphosa wa Afrika Kusini aapishwa kwa muhula wa pili

Cyril Ramaphosa anasema muhula wake mpya kama mwanzo wa enzi mpya.
Cyril Ramaphosa anapongeza muhula wake mpya kama mwanzo wa enzi mpyam| Picha: Reuters

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa alisifu uundaji wa serikali ya muungano mpana kama "mwanzo wa enzi mpya" Jumatano alipokula kiapo kwa muhula wake wa pili kamili.

"Kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa ni wakati wa umuhimu mkubwa. Ni mwanzo wa enzi mpya," alisema Ramaphosa, 71, baada ya uchaguzi mkuu mwezi uliopita kutopata mshindi wa moja kwa moja kwa mara ya kwanza katika miaka 30.

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan  alikuwepo kuhudhuria uapisho wa rais Ramaposha | Picha: Reuters

Ramaphosa alikula kiapo na mkuu wa mahakama ya katiba, Jaji Mkuu Raymond Zondo katika Jengo la Umoja katika mji mkuu, Pretoria.

Wabunge wiki iliyopita walipiga kura kwa wingi kumchagua tena mwenye umri wa miaka 71 baada ya kukubali kuunda kile alichokiita serikali ya umoja wa kitaifa na vyama vingine kadhaa.

Rais wa DRC, Felix Tshisekedi, alikuwepo kuhudhuria uapisho wa rais Ramaposha | Picha: Reuters

Katika muhula wake wa kwanza uchumi ulidorora, ukikumbwa na mgao wa umeme, uhalifu uliendelea kuenea na ukosefu wa ajira uliongezeka hadi asilimia 32.9.

TRT Afrika na mashirika ya habari