Mkutano mkuu wa 60 wa ABU, muungano mkubwa zaidi wa utangazaji duniani uliandaliwa na idhaa ya Utangazaji ya Korea Kusini na kufanyika Seoul kati ya Oktoba 31 na Novemba 1, 2023. Picha/TRT

Mkurugenzi Mkuu wa TRT Mehmet Zahid Sobaci amechaguliwa kuwa rais wa Muungano wa Utangazaji wa Asia-Pasifiki (ABU) kwenye mkutano mkuu wa 60 wa umoja huo.

"Kuchaguliwa kwangu kama rais wa ABU ni muhimu kwa Uturuki la kuwa ni nchi inayoongoza katika nyanja zote," alisema Sobaci, na kuongeza kuwa urais wa ABU ni wa kufurahisha sana kwani unaambatana na maadhimisho ya miaka 100 ya Jamhuri.

Mkutano mkuu wa 60 wa ABU, muungano mkubwa zaidi wa utangazaji duniani wenye takriban watazamaji bilioni 3.5 na wanachama 246 kutoka nchi 65, uliandaliwa na idhaa ya Utangazaji ya Korea Kusini na kufanyika Seoul kati ya Oktoba 31 na Novemba 1, 2023.

"Uturuki lazima iendelee kuinuka na kuimarisha nafasi yake kama taifa linaloongoza. Karne ya Uturuki inahusisha nyanja mbalimbali, ikiwa ni pamoja na siasa za ndani, sera za kigeni, nishati, mazingira, uchumi, viwanda, elimu na teknolojia," Sobaci alisema.

“Kipindi hiki kinaashiria malengo makubwa ya Uturuki, na dhamira yake ya kuyafikia. Kwa hivyo, tunaweza kuuchukulia urais wa ABU kama hatua na mchango katika kufikia malengo ambayo Uturuki imeweka katika sekta ya vyombo vya habari vya kimataifa,” alisema.

‘TRT inahabarisha ulimwengu kuhusu dunia’

Rais huyo mpya wa ABU ambaye pia aliyechaguliwa hivi karibuni na Mkurugenzi Mkuu wa TRT pia alisisitiza umuhimu wa idhaa zinazoendeshwa na Shirika la Utangazaji la Umma la Türkiye, Shirika la Redio na Televisheni la Uturuki (TRT).

“Kwa idhaa kama TRT World na TRT Arabi, pamoja na majukwaa yetu ya kimataifa ya habari za kidijitali, tumebadilika na kuwa taasisi ya utangazaji inayouambia ulimwengu kuhusu ulimwengu,” Sobaci alisema.

“Wakati tunatimiza dhamira hii, hatujapuuza majukumu yetu. Tumejitahidi kuwasilisha maendeleo, migogoro na masuala duniani kote kwa mtazamo wa usawa zaidi,” alisema.

“Tumelenga kuwa sauti ya dhamira ya ulimwengu, sauti ya wale ambao mara nyingi hupuuzwa. Kwa kuzingatia mauaji ya hivi majuzi huko Palestina, tumejitahidi kutekeleza hili kwa vitendo.

Wakati wa uongozi wa Sobaci kama rais wa ABU, TRT itakuwa mwenyeji wa mkutano mkuu wa 61 wa ABU mjini Istanbul, unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2024.

TRT World