Takriban watu 15 wamefariki na wengine kujeruhiwa katika ajali ya basi Mali

Takriban watu 15 wamefariki na wengine kujeruhiwa katika ajali ya basi Mali

Mabasi mawili ya abiria yamegongana na lori la tani 10 lililokuwa limebeba mifugo.
Ajali hiyo ilitokea Jumanne kati ya miji ya Fana na Konobougou kusini mwa nchi. Picha AP

Takriban watu 15 wamefariki na wengine kadhaa kujeruhiwa wakati mabasi mawili ya abiria yalipogongana na lori nchini Mali, mamlaka ilisema.

Ajali hiyo ilitokea Jumanne kati ya miji ya Fana na Konobougou kusini mwa nchi hiyo, alisema Mama Djenepo, katibu mkuu wa wizara ya uchukuzi ya Mali.

"Ajali hiyo ilihusisha mabasi mawili ya abiria yaliyokuwa yakielekea Mopti, ambayo yaligongana na lori la tani 10 lililokuwa limebeba mifugo," alisema na kuongeza kuwa chanzo kinaaminika kuwa mwendo kasi wa madereva waliochoka.

Wakati ajali za barabarani ni za kawaida nchini Mali, haswa wakati wa msimu wa mvua, hii ndiyo mbaya zaidi katika taifa hilo la Afrika Magharibi mwaka huu, serikali ilisema.

Zaidi ya watu 680 waliuawa mwaka jana katika ajali za barabarani na wengine 8,200 kujeruhiwa.

TRT Afrika