Na Coletta Wanjohi
Katika hotuba yake kwa taifa siku ya Jumatano, rais wa Uganda Yoweri Museveni alisema uchumi wa nchi hiyo ni thabiti na mazingira yake ya uwekezaji "yanaendelea kuwa ya ushindani katika eneo hilo na kwingineko".
Anasema changamoto za uchumi bado zinachangiwa sana na athari za mabadiliko ya tabia nchi ambayo yamesababisha ukame katika maeneo ya nchi.
Museveni anasema serikali yake haitatoa ruzuku kwa bei.
"Hatuamini katika kutoa ruzuku kwa matumizi kama vile kutoa ruzuku ya petroli kwa watu kwenda kwenye vilabu vya usiku," alisema wakati wa hotuba bungeni.
"Siwezi kutoa ruzuku ya petroli ili watu waendeshe gari zaidi kwenye vilabu vya usiku, kama wanataka kwenda kwenye vilabu vya usiku wakwende huko kwa gharama zao wenyewe, gharama ya mifuko yao wenyewe."
Museveni anasema anaweza tu kufanya uamuzi wa ruzuku kwa vitu ambavyo bei yake inalazimishwa kuongezeka kwa kuchochewa na ‘mambo yasiyo ya kiuchumi’.
"Hata hivyo kama bei zitapotoshwa na baadhi kama vile vikwazo na nchi za magharibi kwa mfano kutokana na vita kati ya Urusi na Ukraine ambayo imeathiri uzalishaji kama vile mbolea, tunaweza kuwa na mantiki kuangalia ruzuku," anaongeza.
Mzozo wa Russia na Ukraine umekatiza usambazaji wa chakula na mbolea duniani kote na nchi za Afrika zimeathirika.
Museveni anasema serikali yake inaangalia sera zake na huenda "itapata suluhu la kukomesha mataifa ya magharibi kuingilia usambazaji wetu wa mbolea au tunaweza kuangalia kutoa ruzuku kwa angalau mbolea."
Hotuba ya hali ya taifa ilionyesha kuwa uwekezaji wa Kigeni nchini Uganda unaendelea kupata nafuu baada ya kusajili dola milioni 949 katika miezi 6 ya kwanza ya mwaka wa fedha wa 2022/2023.
Serikali ya Uganda inasema kuongezeka kwa uwekezaji kutoka nje kunachangiwa na sera thabiti na nzuri za kiuchumi na amani iliyopo nchini.
Hii pia kwa kiasi inatokana na kuongezeka kwa ufadhili wa sekta ya mafuta na gesi na madini, ukuaji unatokana na uimarishaji wa uchumi wa viwanda vingi, utekelezaji wa mifano kwa biashara ndogo na za kati, kuongezeka kwa shughuli za sekta ya mafuta na gesi.
Uwekezaji wa kigeni kuongezeka pia inachangiwa na ukuaji wa biashara ya kikanda na kuongezeka kwa athari za kuimarika kwa uchumi katika nchi zilizoendelea zinazotoa masoko.
Rais Museveni anasema kuna changamoto kubwa kwani uzalishaji mkubwa unafanyika bila thamani kuongezwa.
Anasema mabadiliko ya kiuchumi yanayotarajiwa yatafanyika ikiwa maswala ya "kushughulikia vibaya wawekezaji, kupoteza muda wao na rushwa" zitamalizwa.