| Swahili
AFRIKA
2 DK KUSOMA
Katika Picha: Vijana waliochoshwa na vita DRC wapata faraja mchezo wa kuteleza
Huku kukiwa na operesheni za kijeshi zinazoendelea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo za kung'oa makundi ya waasi, kijana mmoja anatoa suluhu la kipekee ili kupunguza msongo wa mawazo na kukabiliana na uhalifu mijini
Katika Picha: Vijana waliochoshwa na vita DRC wapata faraja mchezo wa kuteleza
Mchezo wa kuteleza Beni / Others

Licha ya changamoto ya kuwashawishi wazazi kwamba mchezo huo sio hatari sana, wanariadha hao wachanga wa kuteleza wameazimia kuwakilisha Mashariki mwa Kongo kimataifa.

Kundi la Dreams Team Rollers lilianzishwa mwaka wa 2017 baada ya kundi la watoto aliowaona wakiteleza jijini Nairobi, Kenya kumtia moyo Kavuya.

"Niliona kwamba watoto hawa walikuwa na furaha na huru kama ndege... nilijiambia tunahitaji mchezo huu kwa watoto wetu nchini DRC," Kavuya aliiambia TRT Afrika.

Kikundi hicho hakifundishi tu mchezo wa kuteleza kwenye theluji bali pia hutoa ushauri wa kisaikolojia ili kuwasaidia vijana kukabiliana na matatizo ya familia, matumizi mabaya ya dawa za kulevya, na majeraha yanayohusiana na vita.

Kulingana na Kavuya, kuteleza kwenye theluji imekuwa njia ya vijana hao kusahau matatizo yao na kupata furaha ya utotoni.

Justin Mumbere, mcheza michezo yakuteleza mwenye umri wa miaka 19 anasema kwamba kikundi hiki kimebadilisha maisha yake.

“Mwaka mmoja uliopita, nilikuwa na marafiki ambao walikunywa vileo vikali lakini kwa kuwa niko hapa na Dream Team Rollers, nimewaacha wote nyuma,” asema Bw. Mumbere.

"Timu hii ya wanateleza ni kama familia ya pili kwangu - nimebadilisha baadhi ya mawazo," anasema Mumbere.

Kujitolea kwao kumewaletea hadhi ya mashujaa katika eneo la mashariki mwa nchi.

Licha ya mzozo unaoendelea, Joel na wachezaji wake wachanga wa kuteleza wanathibitisha kwamba Mashariki mwa Kongo sio vita tu; kuna maisha na matumaini pia.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Wanigeria wanajiunga na Wakenya, Waghana kama wafanyakazi wanaotafutwa sana na makampuni ya Marekani
Zaidi ya fidia: Mustakbali wa Afrika unahitaji mtazamo mpya sio malipo
Polisi Afrika Kusini wawakamata watu zaidi 1,000 katika msako wa wahalifu
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Congo Makosso ajiuzulu
Watu kumi na nne waliotekwa Nigeria waokolewa: Gavana wa Jimbo
Ziara ya Afrika: Papa Leo afanya Misa nchini Angola
Wamefukuzwa Sahel: Ufaransa inatafuta nini nchini Kenya?
Pande zinazopigana DR Congo zimekubaliana kubadilishana wafungwa na kuruhusu ufikiaji wa msaada
Nigeria yavamia ‘kiwanda cha watoto’ huko Lagos, na kuwaokoa wanawake wajawazito
Marekani yawawekea vikwazo wapiganaji wa Colombia nchini Sudan
Kundi la kwanza la waliofukuzwa kutoka Marekani lawasili Kinshasa nchini DRC
Mtoto wa Mugabe akiri kumtishia mtu kwa bunduki nchini Afrika Kusini
Nigeria yapiga marufuku kusimikwa kwa ‘Wafalme wa Igbo’ nje ya nchi
Mawaziri wa mambo ya nje wa Uturuki, Misri, Pakistan, Saudia kukutana Jukwaa la Diplomasia Antalya
Somalia inasema hatua ya Israel kuunga mkono Somaliland inakiuka Uhuru wa Somalia
Mwakilishi Maalumu wa Jumuiya ya Madola Lazarus Chakwera ahitimisha ziara yake nchini Tanzania
Kenya yaomba msaada wa haraka kutoka Benki ya Dunia huku ikipunguza VAT
Wadau wajadili fursa za uwekezaji katika Kongamano la Biashara linaloendelea Kigoma, Tanzania
Mbunge Tanzania ataka sekta binafsi iruhusiwe uzalishaji wa nishati ya umeme
Kampuni ya BP yashtakiwa Kenya kufuatia madai ya uchafuzi mazingira kutokana na uchimbaji mafuta