Malawi: Watu 26 wauawa baada ya lori la mafuta kugongana na gari ya abiria

Malawi: Watu 26 wauawa baada ya lori la mafuta kugongana na gari ya abiria

Takriban watu 26 wameuawa baada ya matatu kugonga lori la mafuta katikati mwa Malawi siku ya Jumatano.
Gari hilo lilikuwa likijaribu kulipita lori la mafuta, na hatimaye kugongana katikati mwa Malawi mnamo Agosti 21, 2024. / Picha: AA

Takriban watu 26 wameteketea hadi kufa nchini Malawi baada ya matatu kuwaka moto baada ya kugonga lori la mafuta.

Abiria wote waliokuwa kwenye matatu "walichomwa moto kabisa na hakuna aliyenusurika," Harry Namwaza, naibu msemaji wa Huduma ya Polisi ya Malawi, aliiambia Anadolu baada ya tukio hilo lililotokea Jumatano katika wilaya ya Kasungu ya kati.

“Dereva wa gari la abiria alikuwa kwenye mwendo kasi na baadaye kuligonga lori la mafuta katika harakati zake za kutaka kulipita,” alisema Namwaza.

Alisema gari hilo la abiria lilikuwa njiani kuelekea mji mkuu wa nchi hiyo, Lilongwe.

Tabia ya Dereva

Ajali za barabarani hugharimu maisha ya watu wengi kila wiki katika taifa hilo la Kusini mwa Afrika.

Kulingana na ripoti ya Huduma ya Polisi ya Malawi, nchi hiyo ilirekodi ajali 4,977 mwaka jana, zikiwemo 389 kati ya hizo ambazo zilisababisha vifo.

Wikiendi iliyopita, takriban watu kumi waliripotiwa kufariki baada ya gari lililokuwa likiendeshwa kwa kasi kutumbukia sokoni eneo la kusini mwa nchi hiyo.

Viongozi wa Serikali, wahandisi wa barabara na wataalamu wa usalama barabarani wanazihusisha ajali hizo na tabia za madereva na ubovu wa barabara.

TRT Afrika