Mtihani wa KCPE nchini Kenya ulikuwa chini ya mtaala wa 8-4-4, ambao sasa unakatizwa. / Picha: TRT Afrika

Kenya imehitimisha mitihani ya shule ya msingi chini ya mtalaa wa zamani, ambayo wanafunzi walitumia miaka minane shuleni, minne sekondari, na angalau minne chuo kikuu (mtindo wa 8-4-4).

Darasa la 2023, ambalo lilitoa matokeo yake ya mtihani siku ya Alhamisi, lilikuwa la mwisho kupokea alama chini ya mpango wa Cheti cha Elimu ya Msingi cha Kenya (KCPE).

Kuanzia sasa, wanafunzi watakuwa na alama chini ya mfumo mpya wa elimu unaoitwa Mtaala wa Uwezo (CBC), ulioanzishwa Desemba 2017 wakati wa utawala wa aliyekuwa Rais Uhuru Kenyatta.

Chini ya mpango wa CBC, ambao unasisitiza maendeleo ya kitaaluma, kiufundi, na vipaji, wanafunzi watatumia miaka miwili shuleni kabla, miaka sita msingi, miaka mitatu sekondari ya chini, miaka mitatu sekondari ya juu, na angalau miaka mitatu chuo kikuu (mtindo wa 2-6-3-3-3).

Utoaji alama wa kimaendeleo

Tayari, kuna mamilioni ya wanafunzi waliojiandikisha chini ya mtalaa mpya wa elimu.

Wakati wa elimu ya sekondari ya juu (madarasa 10, 11, na 12), wanafunzi wanatarajiwa kuelekeza nguvu (specialise) katika masomo fulani yatakayowawezesha kuingia kwenye taaluma wanayopendelea.

Maeneo makuu ya utaalam, kulingana na serikali ya Kenya, ni Sanaa na Michezo, Sayansi Jamii, na masomo ya STEM (Sayansi, Teknolojia, Uhandisi, na Hisabati).

Tofauti na mfumo wa 8-4-4, ambao una mitihani ya kitaifa mwishoni mwa elimu ya msingi na sekondari, mfumo wa CBC haujajumuisha mitihani ya kitaifa.

Wanafunzi wanapewa alama kwa kimaendeleo, na mkazo zaidi ukiwekwa kwenye ujuzi wa vitendo badala ya nadharia. Mfumo wa CBC pia unaleta ushiriki mkubwa wa wazazi ikilinganishwa na mfumo wa 8-4-4, ambao ulikuwa unaendelea tangu 1985, wakati Daniel Moi alikuwa Rais wa Kenya.

Uratibu wa utendaji

Miaka yote, Kenya imekuwa ikiorodhesha mitihani chini ya mfumo wa 8-4-4, hatua iliyokosolewa na wataalam wa elimu, wakidai kuwa kuorodhesha wanafunzi kunachochea udanganyifu wa mitihani.

Katika taifa la Afrika Mashariki, alama za juu anazopata mwanafunzi, ndivyo nafasi yake ya kujiunga na shule ya sekondari inayopata alama nzuri katika mitihani ya kitaifa ya Cheti cha Elimu cha Sekondari ya Kenya (KCSE) inavyoongezeka.

Chini ya mtaala wa 8-4-4, matokeo ya mtihani wa KCSE yanaamua somo gani mwanafunzi atasomea chuoni, na masomo ya sayansi yanahitaji alama za juu za kufuzu.

Wakati darasa la mwisho la KCPE lilifanya mitihani yake mwaka 2023, darasa la mwisho la KCSE linatarajiwa kufanya mitihani ya kitaifa mwaka 2025.

Mwanafunzi bora wa KCPE mwaka 2023

Chini ya mfumo wa KCPE, wanafunzi wanachukua masomo matano ya mitihani, yaani Hisabati, Kiingereza, Kiswahili, Sayansi, na Masomo ya Jamii/Dini. Kila somo linafaa alama za juu 100, maana yake mtihani wote unapimwa kwa alama 500.

Mwanafunzi bora wa KCPE mwaka 2023 alikuwa Michael Warutere wa Shule ya Riara Springs Academy jijini Nairobi, ambaye alipata alama 428 kati ya alama 500 zinazowezekana.

Kwa KCSE, wanafunzi wanachukua masomo saba yanayopimika, na daraja bora likiwa A sawa na alama 12.

Hii inamaanisha kuwa alama kuu zinazoweza kupatikana katika mtihani wa KCSE ni A safi ya alama 84 (alama 12 za kila somo, zilizochanganywa na saba - idadi kamili ya masomo yanayopimika).

TRT Afrika