Niger, Burkina Faso, Mali waungana kuunda kikosi kitakacho kabiliana na hatari katika ukanda wa Sahel na tishololote kutoka nje / Picha : X - Rais wa Niger

Viongozi wa Mali, Burkina Faso na Niger walitia saini hati ya kuanzisha muungano wa ulinzi, wajumbe wa mawaziri kutoka nchi tatu za Sahel walitangaza katika mkutano na waandishi wa habari. Utiaji saini wa mkataba huo ulifanyika Jumamosi katika mji mkuu wa Mali Bamako.

"Leo, pamoja na Wakuu wa Nchi za Burkina Faso na Niger, nimetia saini Mkataba wa Liptako-Gourma unaoanzisha Muungano wa Nchi za Sahel (AES), ambao lengo lake ni kuanzisha usanifu wa ulinzi wa pamoja na kusaidiana kwa manufaa. ya idadi ya watu wetu", mkuu wa utawala wa kijeshi wa Mali, Assimi Goita, alichapisha kwenye X, mtandao wa kijamii uliojulikana kama Twitter.

Eneo la Liptako-Gourma -- ambapo mpaka wa Mali, Burkina Faso na Niger hukutana -- limeharibiwa na makundi ya waasi wenye silaha katika miaka ya hivi karibuni.

Nchi hizo tatu zinapambana na uasi uliozuka kaskazini mwa Mali mwaka 2012 na kuenea hadi Niger na Burkina Faso mwaka 2015.

Ulinzi na uchumi

Kiongozi wa serikali ya Niger Abdourahmane Tchiani alielezea kutiwa saini kwa mkataba huo kama ''kihistoria'' akisema ''pamoja, tutajenga Sahel yenye amani, ustawi na umoja.''

Kiongozi wa serikali ya Niger Tchiani  alikuwa kwenye hafla ya kutia saini Bamako. Picha: Rais wa du Niger/ X

Nchi zote tatu pia zimepitia mapinduzi tangu 2020, hivi karibuni Niger, ambapo wanajeshi mnamo Julai walimpindua Rais Mohamed Bazoum.

Hivi karibuni nchi hizo zimekuwa na mzozo na jumuiya ya kanda ya Afrika Magharibi, ECOWAS kuhusu mapinduzi yaliyotokea nchini Niger.

ECOWAS ilikuwa imetishia kutumia nguvu kubadili mapinduzi hayo lakini nchi hizo tatu ziliapa kukabiliana na hatua hiyo.

"Muungano huu utakuwa mchanganyiko wa juhudi za kijeshi na kiuchumi kati ya nchi hizo tatu," waziri wa ulinzi wa Mali Abdoulaye Diop alisema katika mkutano na waandishi wa habari Jumamosi.

"Kipaumbele chetu ni mapambano dhidi ya ugaidi katika nchi hizo tatu", aliongeza.

Mvutano na Ufaransa

Mataifa yote matatu yalikuwa wanachama wa kikosi cha pamoja cha G5 Sahel kinachoungwa mkono na Ufaransa na Chad na Mauritania, kilichoanzishwa mwaka 2017 ili kukabiliana na makundi ya Kiislamu katika eneo hilo.

Mali imeachana na shirika hilo butu baada ya mapinduzi ya kijeshi, wakati Rais wa Niger aliyeondolewa madarakani Mohamed Bazoum alisema mwezi Mei mwaka jana kwamba kikosi hicho sasa "kimekufa" kufuatia kuondoka kwa Mali.

Kiongozi wa kijeshi wa Mali Goita aliandaa hafla ya kutia saini huko Bamako. Picha: X - Ikulu ya Rais  Niger

Uhusiano kati ya Ufaransa na mataifa matatu, makoloni yake yote ya zamani, umedorora tangu mapinduzi.

Ufaransa imelazimika kuwaondoa wanajeshi wake kutoka Mali na Burkina Faso, na iko katika mvutano mkali na utawala wa kijeshi ulionyakua mamlaka nchini Niger baada ya jeshi hilo kulitaka liondoe wanajeshi wake na balozi wake.

Mbali na kupambana na waasi wanaohusishwa na Al Qaeda na kundi linalojiita Dola la Kiislamu, Mali imeshuhudia kuanzishwa tena kwa uhasama na makundi yenye silaha ya Tuareg katika wiki moja iliyopita.

Makundi hayo mwaka 2012 yalianzisha uasi kabla ya kutia saini mkataba wa amani na serikali mwaka 2015. Mkataba huo kwa ujumla unachukuliwa kuwa umevunjika.

TRT Afrika