| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Kenya kupunguza bei ya dizeli baada ya maandamano kuhusu ongezeko la gharama ya nishati
Katika hotuba kupitia televisheni, Rais wa Kenya William Ruto amesema kuwa ameagiza bei ya dizeli ipunguzwe kwa shilingi 10 kwa lita (dola 0.0772) katika mzunguko wa bei wa mwezi Juni na Julai.
Kenya kupunguza bei ya dizeli baada ya maandamano kuhusu ongezeko la gharama ya nishati
Upinzani Kenya wametoa wito wa maandamano kupinga kuongezeka kwa bei ya mafuta / Reuters

Rais wa Kenya William Ruto siku ya Ijumaa amesema serikali itapunguza bei ya dizeli katika taifa hilo la Afrika Mashariki ili kuleta ahuweni kwa watu baada ya maandamano kuhusu kuongezeka kwa bei ya nishati kutokana na mapigano Mashariki ya Kati.

Wahudumu wa usafiri wa umma waliandamana mapema wiki hii kwa siku mbili. Watu wanne waliuawa katika maandamano hayo na wengine karibu 30 kujeruhiwa.

Katika hotuba kupitia televisheni, Ruto amesema kuwa ameagiza bei ya dizeli ipunguzwe kwa shilingi 10 kwa lita (dola 0.0772) katika mzunguko wa bei wa mwezi Juni na Julai, ili kuleta ahuweni kwa wananchi.

"Kupitia mpango wa serikali kwa serikali, tumepata hakikisho la kupata mafuta, licha ya kutatizwa kwa usambazaji, kuhakikisha tunapata mafuta kote nchini," Ruto amesema.

Amesema serikali imetumia kiasi kisichopungua shilingi bilioni 28.1 (zaidi ya dola milioni 216) katika hatua za kupunguza bei ya mafuta ikiwemo kuondoa kodi kati ya mwezi Aprili na Juni.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Urusi yaeleza wasiwasi wake kuhusu mlipuko wa Ebola huku Korea Kusini ikitoa tahadhari kwa Uganda
DRC yaongeza uchunguzi wa Ebola katika mji wa Goma unaodhibitiwa na M23
DRC yasitisha mazoezi ya Kombe la Dunia kufuatia hofu ya Ebola
Uganda yakanusha madai ya Marekani ya kufadhili kliniki za Ebola nchini humo
Kesi ya Félicien Kabuga yafutwa rasmi ndani ya Mahakama ya Umoja wa Mataifa
Sierra Leone yakubali kupokea kundi la kwanza la wahamiaji wanaofukuzwa Marekani
Viongozi kadhaa wa Afrika wameipongeza timu ya Arsenal kwa kushinda ubingwa wa EPL
Wanajeshi saba wa Nigeria wauawa katika shambulio la kigaidi
Bahrain yapiga marufuku wageni kutoka DRC, Uganda kwa kuhofia ugonjwa wa Ebola
Rais Samia ataka jamii ielimishwe kuhusu matumizi ya nishati ya nyuklia
Mgomo wa usafiri wa umma Kenya kuhusu kupanda kwa bei ya mafuta wasitishwa
Mjumbe wa zamani wa Ubelgiji anayekabiliwa na kesi ya mauaji ya Patrice Lumumba afariki
Mkenya aliyeacha uhandisi na kujikita kwenye tasnia ya sanaa
Mgomo wa usafiri wa umma nchini Kenya waingia siku yake ya pili, wanne wafariki
Jukwaa la Kidiplomasia la Antalya kwa mtazamo wa viongozi wa Afrika
Tanzania: Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai wa Matukio ya Ghasia Oktoba 29
Ugonjwa wa Ebola waahirisha maadhimisho ya Siku ya Mashahidi wa Uganda
Mwanamke aliyechomwa na moto kwa sababu ya kujichora sura ya Rais Ruto afariki dunia
Rais Mwinyi aishukuru Benki ya Dunia kwa kuendelea kuipatia misaada ya maendeleo Zanzibar
WHO yaanza mkutano wake wa kila mwaka huku kukiwa na tatizo la Ebola DRC