| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Rais Ruto wa Kenya azungumzia changamoto za bei ya mafuta na gharama za maisha
Rais wa Kenya William Ruto amesema kuwa nchi haina uhaba wa mafuta licha ya wasiwasi wa kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo, kutatizika kwa usafiri na hofu kuhusu upatikanaji wa mafuta kutokana na mzozo unaoendelea Mashariki ya Kati.
Rais Ruto wa Kenya azungumzia changamoto za bei ya mafuta na gharama za maisha
Rais wa Kenya William Ruto. / Reuters

Rais wa Kenya William Ruto anasema serikali imepata uhakika wa mafuta kupitia mpango wa serikali kwa serikali, akisisitiza kuwa kwa mkataba wao kimataifa wanaouza mafuta wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanapata bidhaa hiyo nchini.

Akizungumza siku ya Ijumaa katika Ikulu ya Mombasa huku akiangazia tatizo linaloendelea la mafuta, Ruto amesema serikali inafahamu changamoto wanazokabiliana nazo watu za kiuchumi nyumbani, katika biashara na wahudumu wa usafiri wa umma lakini akasisitiza kuwa hali kwa sasa ni shwari.

“Ningependa kuwafahamisha kuwa hakuna uhaba wa mafuta. Kupitia mpango wa serikali kwa serikali, mkataba wetu wa kimataifa tunatakiwa tupate mafuta bila tatizo lolote,” Ruto alisema.

“Serikali inachukua hatua zote kuhakikisha kuwa mafuta yanapatikana."

Rais alikiri kuhusu matatizo ambayo Wakenya wanapitia kufuatia kupanda kwa bei za mafuta, akisema serikali inaelewa changamoto hizo za familia, wafanyakazi na biashara ndogo ndogo kutokana na kupanda kwa gharama za maisha.

“Kwa kila mama ambaye ana wasiwasi kuhusu bei ya vyakula, kila mfanyakazi mwenye wasiwasi kuhusu kama atamudu bei ya nauli akienda kazini kesho, kila mfanyabiashara anayejitahidi kuendeleza biashara yake ndogo, na kila kijana ambaye ana wasiwasi kuhusu mustakabali, nataka mfahamu kuwa serikali ya Kenya inatambua mnayopitia na iko pamoja na nyinyi,” alisema.

Ruto pia alikuwa na ujumbe kwa wahudumu wa usafiri wa umma, wamiliki na wadau katika sekta hiyo ambayo imeathirika pakubwa na kupanda kwa bei ya mafuta.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Urusi yaeleza wasiwasi wake kuhusu mlipuko wa Ebola huku Korea Kusini ikitoa tahadhari kwa Uganda
DRC yaongeza uchunguzi wa Ebola katika mji wa Goma unaodhibitiwa na M23
DRC yasitisha mazoezi ya Kombe la Dunia kufuatia hofu ya Ebola
Uganda yakanusha madai ya Marekani ya kufadhili kliniki za Ebola nchini humo
Kesi ya Félicien Kabuga yafutwa rasmi ndani ya Mahakama ya Umoja wa Mataifa
Sierra Leone yakubali kupokea kundi la kwanza la wahamiaji wanaofukuzwa Marekani
Viongozi kadhaa wa Afrika wameipongeza timu ya Arsenal kwa kushinda ubingwa wa EPL
Wanajeshi saba wa Nigeria wauawa katika shambulio la kigaidi
Bahrain yapiga marufuku wageni kutoka DRC, Uganda kwa kuhofia ugonjwa wa Ebola
Rais Samia ataka jamii ielimishwe kuhusu matumizi ya nishati ya nyuklia
Mgomo wa usafiri wa umma Kenya kuhusu kupanda kwa bei ya mafuta wasitishwa
Mjumbe wa zamani wa Ubelgiji anayekabiliwa na kesi ya mauaji ya Patrice Lumumba afariki
Mkenya aliyeacha uhandisi na kujikita kwenye tasnia ya sanaa
Mgomo wa usafiri wa umma nchini Kenya waingia siku yake ya pili, wanne wafariki
Jukwaa la Kidiplomasia la Antalya kwa mtazamo wa viongozi wa Afrika
Tanzania: Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai wa Matukio ya Ghasia Oktoba 29
Ugonjwa wa Ebola waahirisha maadhimisho ya Siku ya Mashahidi wa Uganda
Mwanamke aliyechomwa na moto kwa sababu ya kujichora sura ya Rais Ruto afariki dunia
Rais Mwinyi aishukuru Benki ya Dunia kwa kuendelea kuipatia misaada ya maendeleo Zanzibar
WHO yaanza mkutano wake wa kila mwaka huku kukiwa na tatizo la Ebola DRC