Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan na Rais wa Iran Ebrahim Raisi kujadili Gaza / Picha: Reuters

Rais wa Iran Ebrahim Raisi anatarajiwa kuwasili Ankara mnamo tarehe 4 Januari kukutana na mwenzake wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan.

Kwa mujibu wa afisa wa Uturuki, mazungumzo kati ya viongozi hao wawili huenda yakazingatia hali huko Gaza na Syria pamoja na uhusiano wa nchi mbili.

Ziara iliyopangwa ya kiongozi wa Iran, Raisi mwishoni mwa Novemba iliahirishwa kwa sababu ya ratiba tofauti za Mawaziri wa Mambo ya Nje wa mataifa hayo mawili, afisa huyo aliongeza.

TRT World