Alibainisha kuwa, kwa kufahamu madhara yatakayotokea kufuatia vitendo vyao, serikali ya Netanyahu imekua na uchokozi zaidi, haswa inapokabiliwa na ukweli. ./Picha: Kumbukumbu ya AA

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Uturuki Fahrettin Altun amesema kuwa wale wanaothubutu kumtishia rais Recep Tayyip Erdogan wanafanya hivyo kwa madhara yao wenyewe, kwani yeye si kiongozi ambae mtu yeyote anaweza kumtisha au kumnyamazisha.

"Rais Erdogan amejitolea maisha yake kupambana na dhuluma na ukatili. Daima amekuwa upande wa wanaoteswa na waliodhulumiwa. Amewaudhi wadhalimu kwa fahari, uthabiti na ukaidi," Altun alisema katika taarifa yake kwenye mtandao wa X siku ya Jumatatu.

Altun alisema kuwa serikali ya Israeli na wajumbe wake wa baraza la mawaziri ni washiriki wa mauaji ya halaiki yanayoendelea Palestina.

"Tayari wamehukumiwa mbele ya maoni ya umma duniani. Ni suala la muda tu kabla ya kuhukumiwa katika mahakama za kimataifa. Watalipia kile walichokifanya," Altun alisema.

Alibainisha kuwa, kwa kufahamu madhara yatakayotokea kufuatia vitendo vyao, serikali ya Netanyahu imekua na fujo zaidi, haswa inapokabiliwa na ukweli.

"Malengo ya mauaji ya halaiki ya serikali ya Netanyahu haiwezi kujadiliwa. Matamshi na vitendo vya wajumbe wa baraza la mawaziri la Israeli vimethibitisha hilo mara nyingi," aliongeza.

'Sitisha mauaji ya kimbari'

Altun alielezea kuwa wawezeshaji wa serikali ya Israeli wanapaswa kuwa na aibu.

Kwa kuwezesha utakaso wa kikabila, walikuwa wakihimiza serikali kuchukua hatua kulingana na silika yake iliyokua mbaya zaidi. Aliongeza kuwa "pongezi za aibu na zisizo na mwisho" kwa Netanyahu katika miji mikuu mbalimbali zinaingiza eneo hilo katika machafuko.

"Ujumbe wetu kwa Israeli uko wazi: Sitisha mauaji ya halaiki na ukubali utawala wa Palestina ikiwa unataka amani na usalama wa kudumu... Huwezi kuficha uhalifu wako wa kivita kwa kumlenga kiongozi wetu," Altun alisema.

Uturuki ni serikali makini na yenye uwajibikaji iliyojizatiti kwa amani na utulivu katika eneo hilo, mkurugenzi wa mawasiliano alisema.

"Hata hivyo, mtu yeyote ambaye ana kichaa cha kutosha kupima mipaka yetu atapata jibu la haraka na thabiti. Kama Uturuki, tumeungana katika suala la Palestina, na hatutamruhusu mtu yeyote kuthubutu kututolea mhadhara au kututisha," taarifa hiyo iliongeza.

TRT World