Saudi Arabia inatarajiwa kuwapokea mahujaji milioni 1.2 wakati wa kipindi cha Hajj, 2024. / Picha: Reuters

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Saudi Arabia imetangaza kwamba wakiukaji wa kanuni na maagizo ya Hajj bila kibali halali wakati wa kipindi cha Hajj wataadhibiwa vikali.

Imesisitiza umuhimu wa kufuata kanuni na maagizo ya Hajj ili mahujaji waweze kutekeleza ibada zao kwa usalama, utulivu na faraja.

Yeyote atakayekapatikana akiwasafirisha wavunjaji wa kanuni na maagizo ya Hajj bila kibali atafungwa kwa kipindi cha hadi miezi sita na kutozwa faini ya hadi riyals 50,000 za Saudi (Dola 13,331).

Wakazi au wenyeji watakaokiuka sheria hizo watahamishwa kwenda nchi zao na kupigwa marufuku kuingia tena katika Ufalme huo, Shirika la Habari la Saudi Arabia limeripoti.

Saudi Arabia inatarajiwa kuwapokea mahujaji milioni 1.2 wakati wa kipindi cha Hajj, 2024.

TRT Afrika na mashirika ya habari