Elon Musk aajiri Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Twitter

Elon Musk aajiri Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Twitter

Ataanza kazi  katika kipindi cha wiki 6 zijazo ,' anasema bilionea Elon Musk
Elon Musk / Photo: AP

Bilionea Elon Musk alitangaza Ijumaa kuwa ameajiri Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Twitter, ambaye atakuwa mrithi wake kuongoza jukwaa la mitandao ya kijamii.

"Nimefurahi kutangaza kwamba nimeajiri Mkurugenzi Mtendaji mpya wa X/Twitter. Ataanza baada ya ~ wiki 6!" Musk aliandika kwenye akaunti yake ya kibinafsi ya Twitter.

"Jukumu langu litabadilika hadi kuwa mwenyekiti mtendaji & CTO, kusimamia bidhaa, programu & sysops," aliongeza, akibainisha kuwa bado atashiriki kikamilifu katika kampuni kama afisa mkuu wa teknolojia (CTO) na kushughulika na uendeshaji wa mifumo.

Alitangaza mnamo Februari kuwa anaweza kuteua Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Twitter kufikia mwisho wa 2023.

Musk pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya kutengeneza magari ya umeme ya Tesla na mtengenezaji wa vyombo vya angani, kizindua, na kampuni ya mawasiliano ya satelaiti ya SpaceX.

AA