Pope / Photo: AA

Papa Francis aliruhusiwa kutoka Hospitali ya Gemelli Jumamosi asubuhi kufuatia kulazwa kwa muda mfupi hospitalini ambako kulihusisha vipimo na matibabu ya bronchitis.

Katika taarifa fupi ya Jumamosi asubuhi, Ofisi ya Waandishi wa Habari ya Holy See ilibainisha kwamba, kabla ya kuondoka kwake, papa alitoa salamu kwa uongozi wa hospitali hiyo, pamoja na timu ya madaktari na wahudumu wa afya waliomsaidia wakati wa kupona kwake.

"Sikuwa na hofu, bado niko hai," papa huyo mwenye umri wa miaka 86 aliwaambia waandishi wa habari na waombaheri nje ya hospitali kabla ya kuondoka.

Waliokuwapo eneo la tukio wanasema alionekana akitabasamu na kupunga mkono kutoka kwenye gari, kabla ya kutoka nje kuzungumza na umati, kisha akaelekea Vatican.

TRT Afrika na mashirika ya habari