Imefanya jumla ya opereshini 1,162 dhidi ya Daesh tangu Juni 1, 2023, polisi wa Uturuki imekamata washukiwa 2,402, waziri amesema. /Picha: Maktaba AA   

Polisi wa Uturuki wamekamata watu 47 wanaoshukiwa kuwa na uhusiano na kundi la kigaidi la Daesh katika miji mikubwa, ikiwemo mji mkuu wa Ankara, na Istanbul, amesema Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki Ali Yerlikaya kupitia mtandao wa X.

Operesheni Bozdogan-6 imefanywa kwa pamoja siku ya Jumatano Adana na Bursa, ikiratibiwa na Kurugenzi ya Usalama wa Taifa na Kitengo cha Kupambana na Ugaidi.

Miongoni mwa waliokamatwa waliohusishwa na Daesh, watu 22 walikamatwa Istanbul, 1 Kirikkale, 15 Ankara, 2 Adana, na 7 Bursa.

Akihimiza dhamira ya amani ya taifa na umoja, Yerlikaya amesema, "Kwa amani, umoja, na mshikamano wa nchi yetu pendwa, hatutawapa nafasi yeyote katika magaidi hao."

'Vita vyetu vitaendelea'

Ameonyesha umuhimu wa jitihada za vikosi vya ulinzi, akisema, "Tutaendelea na mapambano yetu bila kusitishwa kwa jitihada za vikosi vyetu vya ulinzi."

Imefanya jumla ya opereshini 1,162 dhidi ya Daesh tangu Juni 1, 2023, polisi wa Uturuki wamewakamata washukiwa 2,402, waziri amesema.

Uturuki imekuwa nchi ya kwanza kuitaja Daesh kama shirika la kigaidi, imekumbana na mashambulizi kadhaa kutoka kwa kundi hilo.

Zaidi ya waathirika 300 wamepoteza maisha yao, na mamia zaidi wamejeruhiwa katika mauaji 10 ya mabomu ya kujitoa mhanga, na mashambulizi manne ya silaha.

TRT World