Mamlaka ya Uturuki hutumia neno "kumkata makali '' kumaanisha magaidi wanaohusika walijisalimisha au waliuawa au kukamatwa. / Picha: Jalada la AA

Shirika la Kitaifa la Ujasusi la Uturuki (MIT) "limemkata makali " gaidi mkuu wa PKK kaskazini mwa Syria, vyanzo vya usalama vilisema.

Shirika la ujasusi la Uturuki lilimdhibiti Hicran Icuz, aliyepewa jina la Vejin Jiyan, katika operesheni katika mkoa wa Al Hasakah, duru zilisema Jumamosi.

Mamlaka ya Uturuki hutumia neno "kumkata makali " kumaanisha magaidi wanaohusika walijisalimisha au waliuawa au kukamatwa.

Hata hivyo, kundi la kigaidi la PKK limekuwa likisambaza habari za uongo kupitia baadhi ya vyombo vya habari, na kuwapotosha watu kuamini kuwa Icuz alifariki katika ajali.

Icuz, ambaye alijiunga na mrengo wa vijijini wa kikundi hicho mnamo 2016, alipata mafunzo ya kiitikadi na silaha.

Pia aliwafundisha watoto na vijana wa Syria waliojiunga na kundi la kigaidi jinsi ya kutumia silaha na risasi.

Mwanachama huyo wa kigaidi alitekeleza shughuli, hasa katika miundo ya wanawake na vijana wenye silaha ya shirika hilo, na alikuwa miongoni mwa wapangaji wa mashambulizi na shughuli za kimauaju, hasa dhidi ya vikosi vya usalama vya Uturuki katika mikoa ya mpakani.

Magaidi wa PKK mara nyingi hujificha nje ya mpaka, kaskazini mwa Iraq, kupanga mashambulizi.

Katika kampeni yake ya zaidi ya miaka 35 ya ugaidi dhidi ya Uturuki, PKK - iliyoorodheshwa kama shirika la kigaidi na Uturuki , Marekani, na EU - imehusika na vifo vya karibu watu 40,000, ikiwa ni pamoja na wanawake na watoto.

TRT World