Wahanga wa mashambulizi ya jeshi la Israel kwenye nyumba ya familia ya Al-Wasifi karibu na Klabu ya Al-Ahli kwenye kambi ya Nuseirat wakiomboleza katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya Al-Awda mjini Gaza / Picha: AA

Jumatano, Septemba 25, 2024

0233 GMT - Israel imewaua takriban Wapalestina 51, wakiwemo watoto, na kujeruhi wengine kadhaa katika mashambulizi yake ya anga kwenye Gaza iliyozingirwa.

Jeshi la Ulinzi la Raia la Palestina lilitoa taarifa kuthibitisha ukubwa wa uharibifu na hasara iliyosababishwa na mashambulizi ya hivi karibuni ya Israel kwenye eneo lililozingirwa.

Mashambulizi ya jeshi la Israel yalilenga nyumba za makazi, magari mawili, na maeneo ambayo idadi kubwa ya raia walikuwa wamekusanyika, ilisema taarifa hiyo.

0001 GMT - Israel inasema mazungumzo ya kukomboa mateka na Hamas yamegonga mwamba

Mjumbe wa jeshi la Israel katika mazungumzo yenye lengo la kuwaachilia mateka waliokuwa wamezingirwa katika Gaza alionyesha masikitiko yake kuhusu majaribio ya upatanishi kati ya Israel na Hamas.

Jenerali Nitzan Alon alizungumza na familia za Waisraeli waliokuwa mateka huko Gaza na kuwafahamisha kuwa mazungumzo hayo yamefikia mwisho, kwa mujibu wa Idhaa ya 12 ya Israel.

"Kwa sasa, hakuna mpango," aliambia familia, akisema "mapengo ni makubwa sana."

Channel 12 iliripoti kwamba hisia za jumla kati ya familia zilikuwa za kufadhaika na kukata tamaa.

"Familia zimeachwa wakiwa wamekata tamaa, wamechanganyikiwa na wameumizwa," ilisema.

0105 GMT - Ugiriki inasema Israel inapaswa kushinikizwa kusitisha mashambulizi yake huko Gaza

Waziri mkuu wa Ugiriki alisema kuwa mashambulizi ya Israel huko Gaza yanapaswa kukomeshwa haraka iwezekanavyo.

Alipoulizwa katika mahojiano na CNN kama Israel inapaswa kushinikizwa kusitisha mapigano huko Gaza, Kyriakos Mitsotakis alisema: "Nadhani wanatakiwa kushinikizwa kusitisha mapigano. Hivyo ndivyo tunavyohisi, na fursa hizo hazikuchukuliwa."

TRT World