Mkuu wa AU Moussa Faki Mahamat na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ya Kiarabu Ahmed Aboul Gheit walikutana katika mji mkuu wa Misri Cairo Oktoba 15, 2023. / Picha: muungano wa milki za kiarabu

Umoja wa Afrika (AU) na Umoja wa Mataifa ya Kiarabu wamelaani mashambulizi yanayowalenga raia huko Gaza huku mashambulizi ya anga ya Israel yakiendelea katika eneo hilo kufuatia kutokea shambulio la Hamas la Oktoba 7.

"Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Ahmed Aboul Gheit) na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (Moussa Faki Mahamat) wanasisitiza ulazima wa kutoa ulinzi kamili kwa wakazi wa Ukanda wa Gaza," vyombo hivyo viwili vya kanda vilisema katika taarifa ya pamoja.

Gheit na Faki walikutana katika makao makuu ya Jumuiya ya Nchi za Kiarabu katika mji mkuu wa Misri Cairo siku ya Jumapili.

"Wakati wa mkutano huo, pande hizo mbili ziliangazia maendeleo ya matukio huko Gaza, na Katibu Mkuu wa (Ligi ya Nchi za Kiarabu) na Mkuu wa Kamisheni ya (Umoja wa Afrika) walielezea kukataa kwao kabisa mauaji ya raia wasio na hatia," taarifa ya pamoja iliongeza.

Mashambulizi ya anga ya Israel

Gaza imekuwa chini ya mzingiro wa kijeshi wa Israel tangu Oktoba 7, wakati wapiganaji wa Hamas walipoanzisha mashambulizi kusini mwa Israel.

Tangu wakati huo Israel imekata maji, mafuta na usambazaji wa umeme kwa Gaza.

Maelfu ya watu kutoka pande zote mbili wamekufa katika mapigano hayo mapya, huku Gaza ikibeba mzigo mkubwa zaidi.

Jeshi la Israel limewaamuru wakazi wa kaskazini mwa Gaza kuhama kabla ya kuanza mashambulizi ya ardhini.

Mamia ya maelfu ya watu wamekimbia makazi yao huko Gaza, huku miundombinu muhimu kama vile hospitali na shule zikipungua.

Wito wa kujizuia umeongezeka ili kuepusha mateso ya watu kutokana na mapigano.

TRT Afrika