Rais wa Uturuki pia alilaani mashambulizi ya kigaidi nchini Pakistan wakati wa kipindi cha uchaguzi, akisema Uturuki itaendelea kuunga mkono Islamabad katika kupambana na ugaidi. /Picha: AA

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amempongeza rais mpya aliyechaguliwa wa Pakistan, Asif Ali Zardari, ambaye alianza kazi siku ya Jumapili.

Kupitia taarifa kutoka idara ya Mawasiliano ya Uturuki, wakati wa mazungumzo ya simu na Zardari siku ya Jumanne, Erdogan alisema anatarajia uhusiano kati ya nchi hizo mbili kuendelea vizuri katika kila sekta, na kueleza matumaini yake kuwa kipindi kipya kitakuwa na heri kwa Pakistan.

Rais wa Uturuki pia alilaani mashambulizi ya kigaidi nchini Pakistan wakati wa kipindi cha uchaguzi, akisema Uturuki itaendelea kuiunga mkono Islamabad katika kupambana na ugaidi.

Zardari, mwenye umri wa miaka 68, mwenyekiti mwenza wa chama cha kati-kushoto cha Pakistan People's Party, alichaguliwa kama rais wa 14 wa nchi hiyo kwa kipindi cha miaka mitano siku ya Jumamosi.

Mgombea wa muungano tawala alimshinda Mahmood Khan Achakzai, mwanasiasa mkongwe kutoka jimbo la kusini magharibi la Balochistan. Zardari pia alikuwa rais kutoka 2008 hadi 2013.

Pakistan ilifanya uchaguzi mkuu tarehe 8 Februari, ambapo baadaye Shehbaz Sharif alichaguliwa tena kama waziri mkuu.

TRT World