Rais wa Uturuki pia alizitaka nchi zote na mashirika ya kimataifa kuunga mkono kwa dhati mipango inayolenga usitishaji mapigano kwa sababu za kibinadamu katika Gaza ya Palestina / Picha: AA

Uturuki inasisitiza wito wake kwa Israel "kutopanua wigo wa mashambulizi yake dhidi ya raia" na kusitisha operesheni zitakazosababisha "mauaji ya halaiki," Rais Recep Tayyip Erdogan amesema.

"Kwa kuua watoto, wanawake na raia, na kwa kulipua hospitali, shule, misikiti na makanisa kwa mabomu, ni wazi kwamba usalama hauwezi kupatikana," Erdogan alisema katika taarifa yake siku ya Ijumaa kuhusu kuongezeka kwa mzozo kati ya Israel na Palestina.

"Ukandamizaji hauleti amani ya kudumu," alisema kwenye X.

Erdogan aliongeza kuwa eneo hilo lazima likombolewe haraka iwezekanavyo kutokana na "mvurugano wa kichaa wa sasa unaohimizwa na nchi za Magharibi, ambazo vyombo vya habari vya Magharibi vinaonekana kuwa katika mbio za kuhalalisha."

Rais wa Uturuki pia alizitaka nchi zote na mashirika ya kimataifa kuunga mkono kwa dhati mipango inayolenga kufikia haraka usitishaji mapigano wa kibinadamu huko Gaza.

"Tunaamini kwamba kwa kuweka mifumo mipya ya kuhakikisha usalama wa watu wote wanaoishi katika ardhi hizi, eneo letu litapata utulivu wa kudumu," Erdogan alisema.

Rais wa Uturuki pia alisisitiza kuwa Uturuki itaendelea katika juhudi zake za kuzuia vifo vingi vya watu wasio na hatia, kuepusha machafuko zaidi ya kibinadamu, na kutafuta suluhu ya mzozo wa Israel na Palestina "kabla hazijafikia hatua ya kutorejea."

Zaidi ya Wapalestina 4,137 waliuawa

Mzozo katika Gaza ya Palestina, ambayo iko chini ya mashambulizi na vikwazo vya Israel tangu Oktoba 7.

Ulianza wakati Hamas ilipoanzisha Operesheni Al Aqsa Mafuriko, mashambulizi ya kushtukiza ambayo yalijumuisha safu ya kurusha roketi na kujipenyeza ndani ya Israeli kupitia ardhini, baharini na angani.

Imesema uvamizi huo ulikuwa wa kulipiza kisasi kwa kuvamiwa kwa msikiti wa Al Aqsa na kuongezeka kwa ghasia za walowezi wa Israel.

Jeshi la Israel kisha lilianzisha Operesheni ya Upanga wa Chuma dhidi ya maeneo yanayolengwa na Hamas huko Gaza, pamoja na kuongeza mashambulizi na kuwakamata watu katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu.

Mzingiro wa Israel umewaacha wakazi milioni 2.3 wa Gaza na chakula kidogo, maji, mafuta na vifaa vya matibabu.

Takriban Wapalestina 4,137 wameuawa katika mashambulizi ya Israel kwenye eneo la Wapalestina, huku idadi hiyo ikifikia zaidi ya watu 1,400 nchini Israel.

TRT Afrika