Gaidi wa PKK alijiunga na kundi hilo akiwa Ufaransa na kujisalimisha kaskazini mwa Iraq

Gaidi wa PKK alijiunga na kundi hilo akiwa Ufaransa na kujisalimisha kaskazini mwa Iraq

Gaidi huyo alikiri kwamba alikaa katika kambi moja nchini Ugiriki kwa muda kabla ya kutumwa kaskazini mwa Iraq
Mnamo tarehe 22 Juni, wanachama wanne wa PKK waliweka chini silaha zao kwenye vituo vya mpaka vya Uturuki huko Habur na Silopi / Picha: AA 

Mmoja wa magaidi wanne wa PKK, waliotoroka kutoka kwa maficho ya PKK kaskazini mwa Iraq, alijiunga na kundi hilo la kigaidi akiwa nchini Ufaransa, kulingana na Wizara ya Ulinzi ya Kitaifa ya Uturuki.

Gaidi aliyepewa jina la "Munzur B." alijiunga na kundi hilo mwaka jana alipokuwa akiishi Ufaransa na alipelekwa katika kambi za magaidi kaskazini mwa Iraq, wizara hiyo ilisema katika taarifa yake siku ya Jumapili.

Pia alikaa katika kambi huko Ugiriki kwa muda kabla ya kwenda Iraq.

Mmoja wa magaidi wa PKK, ambaye 'alidhibitiwa' kaskazini mwa Iraq wiki iliyopita, alikuwa raia wa Ujerumani.

Gaidi mwingine alijiunga na kundi hilo la kigaidi kutoka Ufaransa.

Mnamo tarehe 22 Juni, wanachama wanne wa PKK waliweka chini silaha zao kwenye vituo vya mpaka vya Uturuki huko Habur na Silopi.

kung'oa ugaidi

Magaidi wa PKK wana maficho kaskazini mwa Iraq, katika mpaka wa Uturuki, wanayotumia kupanga mashambulizi dhidi ya Uturuki.

Ankara imeanzisha msururu wa operesheni za kuwang'oa magaidi waliojificha kaskazini mwa Iraq na kupanga njama za mashambulizi ya mpakani mjini Uturuki.

Katika kampeni yake ya zaidi ya miaka 35 ya ugaidi dhidi ya Uturuki, PKK - iliyoorodheshwa kama shirika la kigaidi na Uturuki, Marekani, na umoja wa Ulaya - imehusika na vifo vya zaidi ya watu 40,000, ikiwa ni pamoja na wanawake na watoto wachanga.

TRT Afrika