Urusi yafanya shambulizi la ndege zisizo na rubani kwenye mji wa Odessa wa Ukraine

Urusi yafanya shambulizi la ndege zisizo na rubani kwenye mji wa Odessa wa Ukraine

Mzozo wa Urusi na Ukraine sasa uko katika siku yake ya 420
Ukraine-Russia conflict / Photo: AFP

Urusi ilizindua shambulio la ndege zisizo na rubani kwenye mji wa bandari wa Odessa ulioko kusini mwa Ukraine mapema Jumatano lakini hakukuwa na ripoti za mara moja za majeruhi, mamlaka ilisema.

"Usiku, adui walifanya shambulio la UAV za aina ya Shahed-136 kwenye mkoa wa Odessa," Yuriy Kruk, mkuu wa utawala wa kijeshi wa wilaya ya Odessa, alisema katika taarifa yake kupitia Telegram.

Kruk alisema ulinzi wa anga wa Ukraine umeharibu ndege nyingi zisizo na rubani lakini baadhi ya miundombinu ya raia iliathirika.

"Kwa mujibu wa taarifa za awali, hakukuwa na majeruhi. Hatua zinachukuliwa kudhibiti moto huo, vitengo vya Huduma ya Dharura ya Serikali na miundo mingine inafanya kazi papo hapo."

Shahed-136 ni ndege ndogo isiyo na rubani iliyotengenezwa na Irani, inayojilipua ambayo inaweza kupangwa kuruka kiotomatiki hadi kwenye seti ya viwianishi vya GPS ikiwa na mzigo wa vilipuzi.

Sekta ya ndege zisizo na rubani nchini Urusi imekubwa na vikwazo vya kimataifa tangu kuanza kwa vita hivyo na kusababisha Moscow kuagiza ndege zisizo na rubani kutoka Iran.

TRT World