Rais Raisi na viongozi wengine waliyofariki katika ajali ya helikopta wanatarajiwa kuzikwa kesho. /Picha: Reuters

Makumi ya maelfu ya Wairani walikusanyika kumuomboleza rais Ebrahim Raisi na wajumbe saba wa msafara wake waliofariki katika ajali ya helikopta kwenye mlima uliofunikwa na ukungu kaskazini magharibi.

Wakipeperusha bendera za Iran na picha za marehemu rais siku ya Jumanne, waombolezaji waliondoka kwenye uwanja wa kati katika mji wa kaskazini-magharibi wa Tabriz, ambako Raisi alikuwa akielekea wakati helikopta yake ilipoanguka siku ya Jumapili.

Walitembea nyuma ya lori lililobeba majeneza ya Raisi na wasaidizi wake saba.

Helikopta yao ilipoteza mawasiliano ilipokuwa njiani kurejea Tabriz, baada ya Raisi kuhudhuria uzinduzi wa mradi wa pamoja wa bwawa kwenye mto Aras, ambao ni sehemu ya mpaka na Azerbaijan, katika sherehe na iliyohudhuriwa na mwenzake wa Azerbaijan Ilham Aliyev.

Operesheni kubwa ya utafutaji na uokoaji ilianzishwa siku ya Jumapili, wakati helikopta nyingine mbili zilizofuatana pamoja na Raisi zilipopoteza mawasiliano na helikopta yake katika hali mbaya ya hewa.

Televisheni ya serikali ilitangaza kifo chake mapema Jumatatu, ikisema "mtumishi wa taifa la Iran, Ayatollah Ebrahim Raisi, amepata kiwango cha juu zaidi cha mauaji ya shahidi," ikionyesha picha zake huku ikisoma Quran.

Waliokufa pamoja na rais wa Iran ni Waziri wa Mambo ya Nje Hossein Amirabdollahian, maafisa wa mkoa na wanachama wa timu yake ya usalama.

Mkuu wa majeshi ya Iran Mohammad Bagheri aliamuru uchunguzi ufanywe kuhusu chanzo cha ajali hiyo huku Wairani katika miji ya nchi nzima wakikusanyika kumuomboleza Raisi na ujumbe wake.

Makumi ya maelfu walikusanyika katika uwanja wa Valiasr wa mji mkuu siku ya Jumatatu.

Maombolezo ya kitaifa

Ali Khamenei, kiongozi mkuu wa Iran na ambaye ana mamlaka ya juu nchini humo, alitangaza siku tano za maombolezo ya kitaifa na kumteua makamu wa rais Mohammad Mokhber, 68, kuwa rais wa mpito hadi uchaguzi wa rais utakapofanyika.

Vyombo vya habari vya serikali baadaye vilitangaza kuwa uchaguzi huo utafanyika Juni 28.

Aliyowakilisha mazungumzo wa masuala ya nyuklia wa Iran Ali Bagheri, ambaye aliwahi kuwa naibu wa Amirabdollahian, aliteuliwa kuwa kaimu waziri wa mambo ya nje.

Kutoka Tabriz, mwili wa Raisi utasafirishwa kwa ndege hadi kituo cha mashekhe wa Kishia cha Qom siku ya Jumanne kabla ya kuhamishiwa Tehran jioni hiyo.

Mikutano yatafanyika katika mji mkuu Jumatano asubuhi kabla ya Khamenei kuongoza sala katika hafla ya kuwaaga.

Mwili wa Raisi utasafirishwa kwa ndege hadi mji alikozaliwa wa Mashhad, kaskazini-mashariki, ambako atazikwa Alhamisi jioni baada ya kukamilika kwa taratibu za mazishi.

Raisi, 63, amekuwa rais tangu 2021.

TRT World