| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Uturuki yakanusha madai kuwa Mkataba wa Ulinzi wa Makkah unakinzana na Kifungu cha 5 cha NATO
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki imesema mkataba huo unaongeza nguvu katika utekelezaji wa majukumu yaliyopo ya ushirikiano wa kiulinzi na si mbadala wa NATO.
Uturuki yakanusha madai kuwa Mkataba wa Ulinzi wa Makkah unakinzana na Kifungu cha 5 cha NATO
"Jitihada za Uturuki za kujenga ushirikiano wa kikanda sio mbadala wa uanachama wake katika NATO," taarifa hiyo ilisema. / / AA

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki imekanusha madai yanayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kwamba Mkataba wa Pamoja wa Ulinzi wa Makkah, uliotiwa saini na Uturuki, Saudi Arabia na Pakistan, unakinzana na Kifungu cha 5 cha Mkataba wa NATO au kwamba unaanzisha muungano mwingine wa kijeshi unaofanana na NATO.

Kifungu cha 5 cha Mkataba wa Muungano wa NATO ni msingi wa ulinzi wa pamoja wa muungano huo, ambapo shambulizi la kijeshi dhidi ya mwanachama mmoja huchukuliwa kuwa ni shambulizi dhidi ya wanachama wote.

Katika taarifa iliyochapishwa Ijumaa kwenye mtandao wa kijamii wa Uturuki wa NSosyal, Kituo cha Kupambana na Upotoshaji wa Taarifa (DMM) kilisema madai hayo ni "ya uongo kabisa" na ni "kampeni ya kupotosha mtazamo wa umma ambayo chanzo chake kinafahamika wazi."

DMM ilieleza kuwa mkataba huo haukinzani na majukumu ya Uturuki katika miungano ya kimataifa iliyopo, ikiwemo wajibu wake ndani ya NATO, bali ni nyenzo inayokamilisha juhudi za kuimarisha usalama wa kikanda.

"Jitihada za Uturuki za kuimarisha ushirikiano wa kikanda si mbadala wa uanachama wake katika NATO," taarifa hiyo ilisema.

Taarifa hiyo iliongeza kuwa Mkataba wa Pamoja wa Ulinzi wa Makkah "si muungano wa kijeshi wenye malengo ya kushambulia, bali ni mfumo wa ulinzi unaolenga kuimarisha uwezo wa kuzuia vitisho."

Kwa mujibu wa DMM, mkataba huo haulengi nchi yoyote wala muungano wowote, bali unalenga kuimarisha ushirikiano katika sekta ya ulinzi, mafunzo ya kijeshi, teknolojia na juhudi za kuimarisha utulivu wa kikanda.

Kituo hicho pia kiliwataka wananchi kuwa na tahadhari dhidi ya "madai yasiyo na msingi na machapisho ya kupotosha."

Taarifa hiyo ilitolewa baada ya Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, kusema mapema Ijumaa kwamba mkataba huo, uliosainiwa mjini Makkah pamoja na Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman na Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif, haulengi nchi yoyote na uko wazi kwa mataifa mengine rafiki yanayotafuta amani, ustawi na utulivu katika eneo hilo.

Erdogan alisema mkataba huo, unaojengwa juu ya kanuni ya kuzuia vitisho kwa pamoja, utaimarisha ushirikiano wa kiulinzi, miradi ya pamoja ya sekta ya ulinzi na juhudi za kupambana na ugaidi, huku ukithibitisha tena dhamira ya Uturuki ya kutatua migogoro kupitia mazungumzo na diplomasia kwa kuzingatia sheria za kimataifa.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Muswada wa “Uturuki Isiyo na Ugaidi” wafungua hatua muhimu katika kukomesha ugaidi: Erdogan
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za amani za Gaza
Uturuki inaweka historia kwa kusafirisha treni ya kwanza iliyotengenezwa nchini humo kwenda Afrika
Mkuu wa shirika la ujasusi wa Uturuki akutana na kiongozi wa Hamas kujadili mpango wa amani wa Gaza
Rais wa Uturuki na Mwana Mfalme wa Saudia wajadili usalama wa kikanda na mpango wa amani wa Gaza
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki na Kuwait wajadili yanayojiri katika kanda
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za kutafuta amani Gaza
Uturuki yalaani mashambulizi ya Israel huko Gaza, ikimtuhumu Netanyahu kwa kuhujumu juhudi za amani
Mpango wa 'Uturuki Isiyo na Ugaidi' kupata msukumo kupitia hatua za bunge: Erdogan
Uturuki na Iraq zasaini makubaliano ya kuongeza matumizi ya bomba la mafuta la Kirkuk-Ceyhan
Uturuki yamkamata gaidi wa FETO aliyekuwa akisakwa kwa jaribio la mwaka 2016 la kumuua Rais Erdogan
Sabiha Gokcen ya Istanbul yaongoza kwa ukuaji wa idadi ya abiria kati ya viwanja vya ndege Ulaya
Uturuki yaimarisha utoaji wa misaada duniani, ikisaidia nchi 85
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Sudan wakutana jijini Ankara
Trump apuuza pingamizi la Netanyahu kuhusu uuzaji wa ndege za kivita za F-35 kwa Uturuki
Erdogan wa Uturuki, Faye wa Senegal wajadili uhusiano, masuala ya dunia
Mwanadiplomasia wa Uturuki Fidan ajadili Kupro, Syria na masuala ya kanda na mkuu wa UN Guterres
Mwanadiplomasia mkuu wa Uturuki Fidan ajadili Cyprus, Syria na masuala ya kikanda na Guterres
Lilikuwa ni jambo la kifahari kuandaa mkutano wa NATO jijini Ankara, asema Erdogan
Waziri wa Sheria wa Uturuki na Saudi Arabia wakutana kuimarisha ushirikiano katika masuala ya sheria