| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Uturuki inaweka historia kwa kusafirisha treni ya kwanza iliyotengenezwa nchini humo kwenda Afrika
Treni hiyo iliyopelekwa Tanzania ilitengenezwa na kampuni ya Uturuki ya vifaa vya reli, Turasas, anasema Waziri wa Uchukuzi wa Uturuki.
Uturuki inaweka historia kwa kusafirisha treni ya kwanza iliyotengenezwa nchini humo kwenda Afrika
Lokomotiv ya kwanza ya Uturuki iliyotengenezwa nchini humo yasafirishwa kwenda Afrika / TRTWorld / TRT World

Treni ya kwanza ya kuvuta mabehewa inayotumia mfumo wa dizeli na umeme na kutengenezwa nchini Uturuki imesafirishwa kwenda Afrika, jambo linaloashiria hatua muhimu katika sekta ya reli ya nchi hiyo.

Waziri wa Uchukuzi, Abdulkadir Uraloglu, alisema katika taarifa yake siku ya Jumatatu kuwa treni hiyo ya aina ya DE 10000 ilitengenezwa na kampuni ya Uturuki ya utengenezaji wa vifaa vya reli, Turasas.

"Tulituma treni yetu ya kuvuta mabehewa aina ya DE 10000 kwenda Tanzania , Treni yetu, ambayo ni matokeo ya uhandisi wa ndani," alisema.

Uraloglu alisema Treni hiyo ilisafirishwa kwenda Tanzania tarehe 29 Julai na itawasili katika Bandari ya Dar es Salaam.

Uraloglu aliongeza kuwa treni hiyo ina injini ya dizeli ya kwanza kabisa kutengenezwa nchini Uturuki yenye nguvu ya zaidi ya farasi 1,000, iliyoundwa kwa ushirikiano kati ya Turasas na Taasisi ya Utafiti wa Kisayansi na Teknolojia ya Uturuki (Tubitak).

"Ujuzi wa kihandisi na uwezo wa usanifu uliopatikana wakati wa utengenezaji wa injini hiyo uliinua kiwango cha uwezo wa kiteknolojia wa Uturuki katika mifumo ya nishati, kwani injini hiyo ni bidhaa muhimu kimkakati inayokidhi mahitaji ya sekta mbalimbali, hasa sekta ya reli," aliongeza.

CHANZO:َAA