| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Uturuki yataka Tunisia kumuachia kiongozi wa chama cha Ennahda
Spika wa Bunge la Uturuki, Numan Kurtulmus, amesema Rached Ghannouchi anahitaji matibabu kufuatia umri wake na hali yake ya afya.
Uturuki yataka Tunisia kumuachia kiongozi wa chama cha Ennahda
"Kwa kuzingatia umri wake na matatizo ya kiafya aliyonayo, uzito wa hali ya Ghannouchi haupaswi kupuuzwa," amesema Kurtulmus. / / Anadolu Agency

Spika wa Bunge la Uturuki, Numan Kurtulmus, siku ya Alhamisi ametoa wito kwa kiongozi wa Harakati ya Ennahda na Spika wa zamani wa Bunge la Tunisia, Rached Ghannouchi, ambaye yuko gerezani, kupewa matibabu na kuachiwa kwa kuzingatiwa utu na ubinadamu.

Kurtulmus amesema kupitia NSosyal, mtandao wa kijamii wa Uturuki, kwamba anafuatilia kwa karibu hali ya Ghannouchi, ambaye amemtaja kuwa “miongoni mwa watu mashuhuri katika mapambano ya amani, demokrasia na mshikamano.”

Amongeza kuwa Ghannouchi amesitisha kugoma kula na kutumia dawa, baada ya kuombwa kufanya hivyo na madaktari wanaofuatilia hali yake.

“Kwa kuzingatia umri wake mkubwa na matatizo ya kiafya aliyonayo, uzito wa hali ya Ghannouchi haupaswi kupuuzwa,” alisema Kurtulmus.

Amemtaja Ghannouchi kuwa mtu aliyejitolea maisha yake kwa “mustakabali wa watu wa Tunisia, uhuru, haki na demokrasia,” akisema licha ya shinikizo, na kuishi uhamishoni na kufungwa, hakuachana na “maadili aliyoyaamini na mapambano yake ya kidemokrasia.”

Kurtulmus amesema Ghannouchi amepata kutambuliwa kwa kiwango kikubwa nchini Tunisia na kimataifa kutokana na “msimamo wake wa kidemokrasia wakati wa kipindi cha mpito, msingi wake imara wa kielimu na mawazo yake.”

“Kwa kuakisi uhusiano wa kina wa kindugu uliopo kati ya watu wa Uturuki na Tunisia, namuombea afya njema na natumaini kwamba atarejea katika hali nzuri ya kiafya haraka iwezekanavyo,” alisema.

“Jambo tunalolitamani zaidi ni kwamba apewe kikamilifu msaada wa matibabu unaohitajika, apewe mazingira ya haki na ya kibinadamu yanayohitajika kwa ajili ya kuheshimu utu wa binadamu, na aachiliwe.”

Kuzuiliwa kwa Ghannouchi

Ghannouchi, ambaye alikuwa Spika wa Bunge lililovunjwa na Rais Kais Saied, amekuwa gerezani tangu alipokamatwa Aprili 17, 2023.

Mahakama iliamuru azuiliwe katika kesi iliyohusiana na matamshi yaliyodaiwa kutolewa na yeye, akishtakiwa kwa “kuchochea dhidi ya usalama wa taifa.” Baadaye alihukumiwa kifungo chaa gerezani katika kesi kadhaa, lakini ameyakataa mashtaka hayo na kusema kuwa yana msukumo wa kisiasa.

CHANZO:Anadolu Agency
Soma zaidi
Erdogan aapa kuipigania dola ya Kipalestina
Rais Erdogan wa Uturuki kukutana na Abbas jijini Ankara kujadili hali ya Palestina
Katika picha: Vivutio mbalimbali vya Uturuki vyang’aa mwanga kushangilia mkataba wa Ulinzi wa Mecca
Rais Erdogan wa Uturuki akutana Kansela Stocker wa Austria
Ndege ya Bayraktar TB2 ya Uturuki yasaidia kudhibiti moto wa nyika nchini Albania
Makubaliano ya Makka ni ya ulinzi wa pamoja lakini hayalengi shabaha au adui yeyote: Waziri Fidan
Uturuki yaadhimisha kumbukumbu ya miaka 59 ya ASEAN na kuahidi kuimarisha ushirikiano wa kikanda.
Uturuki yakanusha madai kuwa Mkataba wa Ulinzi wa Makkah unakinzana na Kifungu cha 5 cha NATO
Mkataba wa Makkah uko wazi kwa mataifa mengine rafiki: Rais Erdogan wa Uturuki
Ukimshambulia mmoja wetu umetushambulia sote, Uturuki, Saudi Arabia na Pakistan wasema
Erdogan kufanya ziara Saudi Arabia atakutana na MBS na Waziri Mkuu wa Pakistan
Mashambulizi ya Israel yanatishia usalama wa Syria: Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki
Muswada wa “Uturuki Isiyo na Ugaidi” wafungua hatua muhimu katika kukomesha ugaidi: Erdogan
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za amani za Gaza
Uturuki inaweka historia kwa kusafirisha treni ya kwanza iliyotengenezwa nchini humo kwenda Afrika
Mkuu wa shirika la ujasusi wa Uturuki akutana na kiongozi wa Hamas kujadili mpango wa amani wa Gaza
Rais wa Uturuki na Mwana Mfalme wa Saudia wajadili usalama wa kikanda na mpango wa amani wa Gaza
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki na Kuwait wajadili yanayojiri katika kanda
Mkuu wa mawasiliano wa Uturuki anasema Israel inahujumu juhudi za kutafuta amani Gaza
Uturuki yalaani mashambulizi ya Israel huko Gaza, ikimtuhumu Netanyahu kwa kuhujumu juhudi za amani