| Swahili
UTURUKI
3 dk kusoma
Uturuki imekamata washukiwa 30 katika operesheni dhidi ya shirika la uhalifu la Alihan Kuris
Kwa mujibu wa ripoti ya Bodi ya Uchunguzi ya Uhalifu wa Fedha, miamala mingi ya kifedha ya shirika hilo imeongezeka baada ya mwaka 2020, huku makampuni yakigawanywa na kuhamishwa
Uturuki imekamata washukiwa 30 katika operesheni dhidi ya shirika la uhalifu la Alihan Kuris
Tathmini ya fedha iliyoandaliwa na Bodi ya Uchunguzi ya Uhalifu wa Fedha (MASAK) kama sehemu ya uchunguzi pia inaangaliwa. / TRT Haber

Vikosi vya usalama ya Uturuki vimekamata washukiwa 30, akiwemo mshukiwa mkuu wa uhalifu Alihan Kuris, katika operesheni inayolenga "shirika la uhalifu la Alihan Kuris," Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu Ankara imesema Alhamisi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ofisi ya Mwendesha Mashtaka, Bodi ya Uchunguzi wa Uhalifu wa Fedha ya Uturuki (MASAK) imeandaa ripoti ya washukiwa na kampuni zinazomilikiwa na shirika la kihalifu kama sehemu ya uchunguzi wa mashtaka ikiwemo "kuanzisha na kuongoza shirika la kihalifu, "uanachama katika shirika la kihalifu,"utakatishaji wa kihalifu,"udanganyifu katika taasisi za umma na mashirika," na "ukiukaji wa Sheria ya Kodi."

Kwa mujibu wa ripoti ya MASAK, idadi ya miamala ya kifedha ya kampuni nyingi zinazomilikiwa na shirika imeongezeka kwa kiwango kikubwa baada ya mwaka 2020, huku kampuni zikihamishwa.

Ripoti hiyo imebaini kwamba kampuni mpya zimeanzishwa na mtaji mkubwa usio wa kawaida na kwamba kampuni mpya zilizoanzishwa zilikuwa katika mikoa tofauti zikifanya kazi katika sekta tofauti na kampuni tanzu.

Baadhi ya kampuni, kwa mujibu wa ripoti, hazikuwa na rasilimali zaidi ya mtaji na hazikuhusika katika biashara hai, isipokuwa kutumia mtaji kutoa ruzuku.

Ripoti hiyo imedai kwamba shirika la kihalifu limetumia mkakati huo kuepuka rekodi za kampuni kufikiwa na kufanya miamala yake kuwa vigumu zaidi kufuatiliwa.

Ripoti hiyo pia imebaini kuwa kampuni nyingi zimepokea miamala kupitia malipo kutoka taasisi mbalimbali na zimekuwa na mzunguko mkubwa wa fedha taslimu, huku wamiliki wa kampuni wakitoa fedha nyingi ambazo chanzo chake kinahitaji maelezo.

Fedha hizo baadae zilitumika na wamiliki kuongeza mtaji.

Imeongeza kusema kuwa kiwango kikubwa cha fedha kimewekwa katika akaunti za kampuni zilihamishwa kwa kampuni chini ya uchambuzi kwa namna ya kipekee, huku kiwango kikubwa cha fedha kimepokewa kupitia malipo ya taasisi na kuwekwa katika fedha taslimu katika kampuni kadhaa.

Ripoti imeonesha manunuzi na mauzo ya kampuni yalikuwa ya kiwango cha juu na mashirika mengine ya kisheria, na kuongeza kwamba, miamala hiyo ilikuwa ya kuzingatiwa katika utoaji wa ankara za kubuni.

Pia imebaini miamala ya fedha za kigeni kutoka kampuni kadhaa za nje ambazo rekodi zake hazikuoana, huku baadhi ya kampuni zikipokea marudisho makubwa ya kodi.

Kama sehemu ya uchunguzi, operesheni za pamoja zinazolenga shirika la uhalifu la Alihan Kuris zilifanyika katika mikoa 17, hasa Istanbul, Ankara na Antalya.

Mamlaka zimetoa vibali vya kukamatwa kwa washukiwa 49, miongoni mwao wakiwa nje ya nchi, pamoja kibali cha kukaguliwa kwa anuani 43 zinazomilikiwa na washukiwa na anuani 80 zinazomilikiwa na kampuni 33.

Katika washukiwa 49, 30, akiwemo Alihan Kuris, walikamatwa katika operesheni. Tisa wako nje ya nje, huku jitihada zikiendelea kuwakamata 10 waliobaki.