| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Mwanadiplomasia wa Uturuki Fidan ajadili Kupro, Syria na masuala ya kanda na mkuu wa UN Guterres
Katika mazungumzo kwa njia ya simu, pande zote mbili zilijadili kuhusu yanayojiri Mashariki ya Kati na Mashariki mwa Mediterania huku Katibu Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa akijiandaa kutembelea kisiwa cha Kupro.
Mwanadiplomasia wa Uturuki Fidan ajadili Kupro, Syria na masuala ya kanda na mkuu wa UN Guterres
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres wamejadili masuala ya kanda.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan siku ya Jumapili alijadili masuala yanayojiri katika kanda kwa njia ya simu na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.

Kulingana na vyanzo vya Kidiplomasia vya Uturuki, Fidan na Guterres walijadili yanayojiri katika kanda kwa kuzingatia ziara ya mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa nchini Syria na kisiwa cha Kupro.

Umoja wa Mataifa utawasilisha ripoti kamili kwa Baraza la Umoja wa Mataifa baadaye mwezi huu kuhusu ukiukaji wa Israel nchini Syria, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres alisema siku ya Jumapili.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Damascus, Guterres alisisitiza kuwa ukiukwaji wa uhuru wa Syria “haukubaliki,” akitoa wito kwa Israel kuheshimu Makubaliano ya 1974.

“Kumekuwa na ukatili nchini Syria lakini bado haujawavunja moyo watu wa Syria kuendelea na maazimio yao,” aliongeza.

Alionya kuwa misaada ya Umoja wa Mataifa kwa watu inafikia mahitaji ya karibu asilimia 20 pekee ya watu wa Syria.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres aliwasili jijini Damascus siku ya Jumamosi kwa ziara ya siku tatu na kufanya mazungumzo na Rais Ahmed al Sharaa na Waziri wa Mambo ya Nje Asaad al Shaibani, wakati ambao alisisitiza dhamira ya Umoja wa Mataifa kuhusu uhuru wa Syria, pamoja na mipaka yake na kutoa wito kwa jamiii ya kimataifa kuunga mkono ujenzi mpya wa nchi hiyo.

Umoja wa Mataifa umetangaza siku ya Alhamisi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ataelekea Kupro kupigia chapuo mchakato wa amani.

"Katibu Mkuu atasafiri kwenda Kupro kuanzia Julai 27 hadi Julai 29 kama sehemu ya utendaji wake kazi na dhamira thabiti kwa suala la Kupro," msemaji wake Stephane Dujarric alisema wakati wa mkutano na waandishi wa habari.

Akieleza kuwa Guterres atakutana na Rais wa Taifa la Uturuki la Kupro Kaskazini (TRNC) Tufan Erhurman na Nikos Christodoulides, kiongozi wa Kupro Kusini inayosimamiwa na Ugiriki, Dujarric alisema kuwa mkuu wa Umoja wa Mataifa pia atakutana na "wadau wengine na kujadili juhudi za kuimarisha mchakato wa amani na kuunga mkono usalama katika kisiwa hicho, ikiwemo kutathmini majukumu ya vikosi vya amani vya Umoja wa Mataifa, UNFICYP."

CHANZO:َAA