| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Uturuki yamkamata gaidi wa FETO aliyekuwa akisakwa kwa jaribio la mwaka 2016 la kumuua Rais Erdogan
Mshukiwa huyo, ambaye ni Kapteni wa jeshi la wanamaji aliyefutwa kazi na rubani wa zamani wa helikopta, alikuwa akisakwa chini ya Ilani Nyekundu ya Interpol.
Uturuki yamkamata gaidi wa FETO aliyekuwa akisakwa kwa jaribio la mwaka 2016 la kumuua Rais Erdogan
Mshukiwa huyo, aliyetambuliwa kama BK, alikuwa sehemu ya kundi la FETO lililohusika katika jaribio la kumuua Rais Erdogan. / AA

Wizara ya Mambo ya Ndani imesema polisi wa Uturuki wamemkamata mwanachama wa kundi la kigaidi la FETO ambaye alikuwa akisakwa kwa kuhusika katika jaribio la kumuua rais wakati wa jaribio la mapinduzi lililoshindwa mwaka 2016.

Wizara hiyo ilisema Jumamosi kuwa mtuhumiwa huyo, anayetambulika kwa herufi za awali BK, alikuwa sehemu ya kikosi cha Shirika la Kigaidi la Fetullah (FETO) kilichohusika katika jaribio la kumuua Rais Recep Tayyip Erdogan huko Marmaris wakati wa jaribio la mapinduzi la Julai 2016.

Wizara ilieleza kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa Kapteni katika jeshi la wanamaji aliyefukuzwa kazi na rubani wa zamani wa helikopta, ambaye alikuwa akisakwa chini ya 'Ilani Nyekundu' ya Interpol.

Kwa mujibu wa wizara hiyo, vitengo vya ujasusi vya polisi katika mikoa ya Afyonkarahisar na Eskisehir vilifanya operesheni ya pamoja iliyoratibiwa na Idara ya Ujasusi ya Kurugenzi ya Usalama.

Operesheni hiyo ilimtambua mtuhumiwa huyo, anayejulikana kama BK, ambaye baadaye alikamatwa na polisi wa kupambana na ugaidi huko Afyonkarahisar, wizara ilisema.

Wizara ilisema Uturuki itaendelea na mapambano yake dhidi ya FETO na mifumo yake.

Jaribio hilo la mapinduzi lililoshindwa, ambapo watu 253 waliuawa na 2,734 kujeruhiwa, lilipangwa na kutekelezwa na FETO chini ya kiongozi wake mkuu, Fetullah Gulen.

CHANZO:َAA