| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Jamhuri ya Afrika ya Kati yafunga mgodi wa dhahabu baada ya watu kufariki
Juhudi za uokoaji zilisitishwa kutokana na mgodi kutitia na mvua kubwa inayoendelea kunyesha.
Jamhuri ya Afrika ya Kati yafunga mgodi wa dhahabu baada ya watu kufariki
Mgodi kama huo wa dhahabu wa Be-Mbari, pia karibu na mpaka wa Cameroon, ulisababisha vifo vya watu kadhaa mwezi Juni.

Jamhuri ya Afrika ya Kati imefunga kwa muda mgodi wa dhahabu karibu na mpaka wa Cameroon baada ya maporomoko ya ardhi kusababisha vifo vya watu kadhaa mapema wiki hii, waziri wa madini wa nchi hiyo alisema siku ya Alhamisi.

Rufin Benam-Beltoungou alitembelea mgodi wa Zamboye siku ya Jumatano na kueleza kuwa idadi rasmi ya waliofariki ni 49, wizara iliiambia AFP.

Waziri huyo alithibitisha kuwa watu hao ni pamoja na raia wa Jamhuri ya Afrika ya Kati 34, 13 kutoka Cameroon na raia wawili wa Chad.

Vyanzo kadhaa vya eneo hilo viliiambia AFP kuwa watu karibu walifariki, huku wakiwa hawajulikani waliko na pengine wamefukiwa na kifusi.

Watu saba waliojeruhiwa walipelekwa katika hospitali ya karibu ya mji wa Baboua, karibu umbali wa kilomita 50.

Maafisa wa usalama wanalinda migodi

Mgodi huo ulikuwa umefungwa na watu walizuiwa kufika huko siku ya Alhamisi, mwandishi wa AFP aliripoti.

Maafisa zaidi wa usalama walipelekwa, ikiwemo wale kutoka kundi la wapiganaji la Urusi la Wagner.

Juhudi za uokoaji zilisitishwa kutokana na kuendelea kutitia kwa mgodi na mvua kubwa kuendelea kunyesha.

Waziri wa madini anasema mkasa huo unadhihirisha hatari za uchimbaji haramu wa madini, "hasa katika maeneo ambayo yana viwango vidogo vya usalama".

Kuporomoka kwa migodi katika taifa la Jamhuri ya Afrika ya Kati hutokea mara kwa mara, ambapo kuna dhahabu na madini mengine yanayochimbwa kwa njia haramu na serikali haina utaratibu wa kuratibu.

CHANZO:TRT Afrika Swahili