| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Wadau wajadili fursa za uwekezaji katika Kongamano la Biashara linaloendelea Kigoma, Tanzania
Waziri Mkuu amesema makongamano ya aina hiyo yana mchango mkubwa katika kuimarisha ushirikiano miongoni mwa mataifa yanayoshiriki.
Wadau wajadili fursa za uwekezaji katika Kongamano la Biashara linaloendelea Kigoma, Tanzania
Waziri Mkuu amesema makongamano ya aina hiyo yana mchango mkubwa katika kuleta ushirikiano. Picha/PMO / TRT Afrika Swahili

Waziri Mkuu wa Tanzania Mwigulu Nchemba amewahimiza viongozi na watendaji wa Serikali kuweka mikakati madhubuti ya kuimarisha usalama wa kikanda ili kuchochea uwekezaji wa kikanda na kimataifa.

Waziri Mkuu ameyasema hayo Alhamisi, Aprili 16, 2026 mkoani Kigoma wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Biashara na Uwekezaji la Ziwa Tanganyika, linalofanyika kwa siku nne mjini Kigoma.

Kongamano hilo ambalo linawakutanisha viongozi wa Serikali, wafanyabiashara na wawekezaji kutoka nchi zinazozunguka Ziwa Tanganyika zikiwemo Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Tanzania ambayo ni mwenyeji.

Waziri Mkuu amesema makongamano ya aina hiyo yana mchango mkubwa katika kuimarisha ushirikiano miongoni mwa mataifa yanayoshiriki.

“Tuna imani kuwa kongamano hili litaibua matumaini mapya ya ushirikiano wa Ukanda wa Ziwa Tanganyika,” amesema Waziri Mkuu.

“Ukanda huu ndiyo unaongoza kwa madini adimu duniani, na dunia ipo kwenye mwelekeo wa matumizi ya madini haya, hivyo sisi ni matajiri wa madini hayo na hatuna budi kuimarisha ushirikiano ili madini hayo yawanufaishe wananchi. Hivyo ni muhimu kushirikiana kuimarisha na usalama wa ukanda huu; na makongamano kama haya yanachangia pakubwa kuboresha ushirikiano huo kwenye nyanja zote,” amesema.

Waziri Mkuu amesisitiza kuwa mkoa wa Kigoma una fursa na rasilimali nyingi ambazo bado hazijatumika ikiwemo ardhi kubwa yenye rutuba, vivutio vya utalii, madini na viwanda vinavyotoa nafasi ya kuchochea uwekezaji mkoani humo.

Kwa upande wake, Gavana wa Jimbo la Tanganyika la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Christian Kifungwa Muteba ameishukuru Serikali kwa kuendelea kushirikiana na nchi hiyo katika nyanja mbalimbali ikiwemo ulinzi na usalama.

Amesema kuwa uwekezaji wa bandari kubwa katika Ziwa Tanganyika utarahisisha usafirishaji wa madini adimu kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwenda nchi nyingine bila kulazimika kupitia katika mataifa yaliyo mbali na nchi hiyo.

Soma zaidi
Wanigeria wanajiunga na Wakenya, Waghana kama wafanyakazi wanaotafutwa sana na makampuni ya Marekani
Zaidi ya fidia: Mustakbali wa Afrika unahitaji mtazamo mpya sio malipo
Polisi Afrika Kusini wawakamata watu zaidi 1,000 katika msako wa wahalifu
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Congo Makosso ajiuzulu
Watu kumi na nne waliotekwa Nigeria waokolewa: Gavana wa Jimbo
Ziara ya Afrika: Papa Leo afanya Misa nchini Angola
Wamefukuzwa Sahel: Ufaransa inatafuta nini nchini Kenya?
Pande zinazopigana DR Congo zimekubaliana kubadilishana wafungwa na kuruhusu ufikiaji wa msaada
Nigeria yavamia ‘kiwanda cha watoto’ huko Lagos, na kuwaokoa wanawake wajawazito
Marekani yawawekea vikwazo wapiganaji wa Colombia nchini Sudan
Kundi la kwanza la waliofukuzwa kutoka Marekani lawasili Kinshasa nchini DRC
Mtoto wa Mugabe akiri kumtishia mtu kwa bunduki nchini Afrika Kusini
Nigeria yapiga marufuku kusimikwa kwa ‘Wafalme wa Igbo’ nje ya nchi
Mawaziri wa mambo ya nje wa Uturuki, Misri, Pakistan, Saudia kukutana Jukwaa la Diplomasia Antalya
Somalia inasema hatua ya Israel kuunga mkono Somaliland inakiuka Uhuru wa Somalia
Mwakilishi Maalumu wa Jumuiya ya Madola Lazarus Chakwera ahitimisha ziara yake nchini Tanzania
Kenya yaomba msaada wa haraka kutoka Benki ya Dunia huku ikipunguza VAT
Mbunge Tanzania ataka sekta binafsi iruhusiwe uzalishaji wa nishati ya umeme
Kampuni ya BP yashtakiwa Kenya kufuatia madai ya uchafuzi mazingira kutokana na uchimbaji mafuta
Mashirika ya ndege ya Nigeria yatishia kusitisha huduma kuanzia Aprili 20 kutokana na bei ya mafuta