| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Mashirika ya ndege ya Nigeria yatishia kusitisha huduma kuanzia Aprili 20 kutokana na bei ya mafuta
Mashirika ya ndege ya Nigeria yatasitisha huduma zote kuanzia Aprili 20 kama bei ya mafuta haitapunguzwa, Shirika la Wafanyabiashara wa ndege la Nigeria (AON) lilisema siku ya Alhamisi.
Mashirika ya ndege ya Nigeria yatishia kusitisha huduma kuanzia Aprili 20 kutokana na bei ya mafuta
Mashirika ya ndege ya Nigeria yametishia kusitisha huduma kuanzia Aprili 20, 2026, kutokana na kuongezeka kwa bei ya mafuta. / Reuters
tokea masaa 2

Mashirika ya ndege ya Nigeria yatasitisha huduma zote ifikapo Aprili 20 kama bei ya mafuta ya ndege haitapunguzwa, Shirika la Wafanyabiashara wa ndege la Nigeria (AON) lilisema siku ya Alhamisi.

Shirika hilo, ambalo linajumuisha wafanyabiashara kadhaa wa ndege za ndani ya nchi, limetuma barua kwa Shirika la Masoko ya Nishati la Nigeria (MEMAN) Aprili 14, likilalamika kuhusu kupanda kwa bei za mafuta ya ndege kwa karibu asilimia 270% tangu mwishoni mwa mwezi Februari.

'Fedha hazitoshi kulipia gharama ya mafuta'

"Sasa hivi, mapato kutoka kwa mashirika ya ndege hayatoshi kulipia gharama za mafuta ya ndege pekee," barua hiyo ilisema.

Bei za juu za mafuta ya ndege zimeharibu sekta ya ndege duniani ikiwa ni matokeo ya vita vya Iran, na kulazimisha mashirika ya ndege kuongeza nauli, kusitisha mipango ya ukuaji na kutafakari kuhusu mustakabali.

Lakini mashirika ya barani Afrika yako hatarini zaidi, huku ongezeko la bei ya mafuta likiwa kati ya asilimia 30% na 40% ya gharama za uendeshaji biashara, ikilinganishwa na duniani ambapo gharama hizo ni wastani wa asilimia 20% na 25%, kulingana na Shirika la Wafanyabiashara wa Ndege Afrika.

zaidi ya lita milioni 2 kila siku

AON inasema kuwa ongezeko la nauli linaweza kupunguza idadi ya abiria nchini Nigeria, huku kufunga kabisa shughuli za ndege kunaweza kuwa na athari kubwa zaidi, ikiwemo watu kupoteza kazi.

Sekta ya ndege ya Nigeria ilitumia lita milioni 2.1 ya mafuta kwa siku mwezi uliopita, takwimu kutoka kwa shirika la taifa la kuratibu mafuta zinaonesha.

Hata hivyo, Kiwanda cha kusafisha mafuta cha Dangote – ambacho peke yake ndiyo kinazalisha mafuta ya ndege nchini Nigeria – hakikusambaza mafuta yoyote katika soko la nyumbani mwezi Machi, takwimu zinaonesha.

CHANZO:TRT Afrika Swahili