Na Cindy Kasanga
Vijana barani Afrika wameitwa kuwa raslimali kubwa lakini kauli hiyo imepoteza maana. Rasilimali zinatakiwa kuhusishwa katika uwekezaji — lakini nani anafaidi wakati hilo linakuwa halifanyiki?
Idadi ya vijana barani Afrika inatazamiwa kuongezeka kwa milioni 132 muongo huu. Idadi kubwa ya vijana siyo sehemu ya mkakati.
Sababu ni ya kisiasa. Uchumi wa mataifa ya Afrika, kama ilivyo kwa mifumo ya sasa hivi, hayatoi fursa kwa vijana wake kuchangia katika kazi zenye tija. Wengi wanatengwa katika maeneo ya kutoa maamuzi.
Maandamano ya hivi majuzi ya vijana yalidhihirisha tatizo hili. Nchini Kenya,maandamano dhidi ya Muswada wa Fedha ambao uliongeza kodi kwa bidhaa za misingi yalionesha ghadhabu kwa serikali ambayo iliahidi ahuweni lakini ikaishia kuwapa watu dhiki.
Nchini Madagascar, kukatika kwa umeme na kukithiri kwa umaskini kulifanya vijana waingie barabarani kutaka mabadiliko. Huko Morocco, hasira za vijana ni kuhusu fedha kidogo kwa ajili ya shule na hospitali huku serikali ikianikwa kwa kulipa kipaumbele suala la viwanja kuliko huduma za kijamii. Kote barani, upinzani wa vijana unaonesha jambo moja: kutengwa kwao kisiasa.
Vijana hawana nafasi
Kwa kuwa tabaka za wazee ndilo limejikita zaidi kwenye siasa, ikiwa ni muenendo uliokuwepo tangu kuondoka kwa wakoloni. Pamoja na serikali nyingi kuahidi kujumuisha vijana, lakini hali ni tofauti.
Wakati huo huo, ufisadi unaendelea kumaliza rasilimali ambazo zingesaidia kubadilisha maisha ya vijana. Afrika inapoteza Dola bilioni $9 kila mwaka kwa tatizo la usimamizi mbaya wa fedha — pesa ambazo zingetumika kufadhili shule, ajira, na miundombinu ambayo vijana wengi wanataka. Ufisadi unasababisha hali ya kutojali, kudhoodisha taasisi, na kuondoa uaminifu kati ya serikali na raia.
Kiuchumi, hali ni mbaya. Sekta isio rasmi inasaidia karibu asilimia 70% ya familia barani Afrika na kutoa ajira kwa vijana. Mara nyingi kazi hizi zinakuwa si za kudumu, na mshahara wake ni mdogo. Asilimia tisini ya vijana wanafanya kazi katika sekta isiyo rasmi, na thuluthi moja wanaishi katika hali ya umaskini licha ya kuajiriwa. Kwa kifupi, kuwa kazi siyo hakikisho la kuondokana na umaskini.
Wakati wa kujumuishwa sasa
Maandamano yaliyokuwepo kote barani siyo tu ni jambo la kupita lakini ni mitazamo kwa serikali ambazo zinazungumzia kuhusu uwezo wa vijana bila ya kutekeleza. Baadhi ya vijana wameuawa wakitetea haki hii — jambo lisilokubalika katika jamii inayodai kuhesimu mustakabali wao.
Vijana wa Afrika siyo tu wanasubiri sera zipitishwe; wanatoa muelekeo katika bara kupitia uanaharakati, ujasiriamali, na umoja. Swali si kuwa kama vijana wako tayari. Ni kama viongozi barani Afrika wako tayari.
kinachotakiwa kufanywa: marekebisho katika uchumi ambao unawaweka vijana katika hatari, na kukasimu mamlaka ili wasiwe kimtya. Vipaumbele viwili hivi haviwezi kutenganishwa.
Kwa muda mrefu vijana wameahidiwa fursa. Ni wakati wa utekelezaji sasa.
Mwandishi, Cindy Kasanga, ni mtafiti anayesoma Shahada ya Uzamili ya Sayansi ya Siasa katika Chuo Kikuu cha British Columbia. Amezaliwa na kulelewa nchini Kenya na Ethiopia, utafiti wake unaangazia suala la usawa, madaraka, na mfumo wa taasisi katika uhusiano wa kimataifa, akiangazia barani Afrika.









