| Swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Erdogan wa Uturuki asisitiza kuunga mkono uhuru wa Sudan katika mazungumzo na Waziri Mkuu Idris
Viongozi hao wawili wamejadili uhusiano wa mataifa yao na kuhusu mapigano yanayoendelea nchini Sudan, kuahidi kuongeza misaada kwa watu na kuunga mkono juhudi za kidiplomasia katika kurudisha hali ya usalama.
Erdogan wa Uturuki asisitiza kuunga mkono uhuru wa Sudan katika mazungumzo na Waziri Mkuu Idris
Mkutano huo uliangazia uhusiano kati ya Uturuki na Sudan, pamoja na masuala ya kikanda na ulimwenguni. / AA

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amemlaki Waziri Mkuu wa Sudan Kamil Idris, ambaye yuko katika ziara ya kikazi nchini Uturuki, kwenye Ikulu ya Rais jijini Ankara, kulingana na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki.

Mkutano huo wa Jumatano uliangazia uhusiano kati ya Uturuki na Sudan, pamoja na masuala ya kikanda na ulimwenguni, kurugenzi ilisema katika mtandao wa kijamii wa Uturuki NSosyal.

Erdogan amesema nchi hizo mbili zinalenga kuimarisha uhusiano kupitia hatua za sasa na zile za mustakabali, akisisitiza kuwa Uturuki itaendelea kuunga mkono uhuru wa Sudan na mipaka yake.

Rais wa Uturuki pia alisema kuwa Uturuki inajitahidi kusaidia katika kumaliza mapigano nchini Sudan na kurudisha hali kuwa ya kawaida, akiongeza kuwa Uturuki inaunga mkono juhudi za kidiplomasia kusitisha mapigano na kuanzisha mchakato kamili wa kisiasa.

Erdogan alieleza kuwa misaada inayolenga kuwapunguzia matatizo watu wa Sudan itaendelea katika kipindi hiki.

Mkutano huo pia ulihudhuriwa na Makamu wa Rais wa Uturuki Cevdet Yilmaz, Waziri wa Mambo ya Nje Hakan Fidan, Waziri wa Nishati na Maliasili Alparslan Bayraktar, Waziri wa Kilimo na Misitu Ibrahim Yumakli, na Mkurugenzi wa Mawasiliano Burhanettin Duran.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Erdogan ampokea Waziri Mkuu wa Singapore jijini Istanbul
Uwanja wa Ndege wa Sabiha Gokcen jijini Istanbul wa kwanza kwa kuzingatia ratiba Ulaya
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan akutana na Vladimir Putin mjini Kazan
Kesi ya Marekani dhidi ya Halkbank yatupiliwa mbali baada ya miaka tisa
Ripoti ya Bunge la Ulaya 'ina upendeleo' na 'haina ukweli': Uturuki
Fidan wa Uturuki ahimiza 'upitishaji salama, bure na bila kukatishwa' katika mazungumzo na Lavrov
Somalia imepokea vifaa vya kisasa kutoka Uturuki kukuza ukulima
Uwanja wa ndege mpya wafunguliwa katika mji mkuu wa Uturuki kabla ya mkutano wa NATO
Mashambulizi ya Israel nchini Syria na Lebanon yanaihatarisha Uturuki, asema Rais Erdogan
Mkakati wa Uturuki wa ‘kutokomeza chanzo cha ugaidi’ unaonyesha mafanikio: Erdogan
Miaka 22 baadaye: Je, Uturuki inaweza kurudia maajabu ya 2002 katika Kombe la Dunia 2026?
Rais Erdogan amejadili uhusiano wa pande mbili, masuala ya kimataifa na Rais Rodriguez wa Venezuela
Amani nchini Ukraine ni muhimu kwa usalama na utulivu wa kikanda: Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki
Uturuki na India waweke 'tofauti zao kando' na kuangazia agenda chanya: Fidan
Emine Erdogan: Taka Sifuri nguzo muhimu ya hatua ya kuhimili mabadiliko ya tabia nchi
Nini kitarajiwe kutoka kwa ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan nchini Bangladesh
Trump kuhudhuria 'mkutano muhimu' wa NATO nchini Uturuki: Rubio
Uturuki, Armenia wafanya mkutano wa biashara Kars kuimarisha uhusiano wa kiuchumi
Spika wa bunge la Uturuki ashtumu UN kutokuwa 'thabiti' katika kuzuia migogoro
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Hakan Fidan awasili Indonesia ili kuimarisha uhusiano wa kibiashar