| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Mashambulizi ya Israel nchini Syria na Lebanon yanaihatarisha Uturuki, asema Rais Erdogan
Rais wa Uturuki, Erdogan, ameitaka jumuiya ya kimataifa kuizuia Israel kutoendelea kuhatarisha utulivu wa dunia.
Mashambulizi ya Israel nchini Syria na Lebanon yanaihatarisha Uturuki, asema Rais Erdogan
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan akiwasalimia wafuasi wake wakati wa mkutano wa chama cha AK Party bungeni jijini Ankara Juni 10, 2026. / / AA

Rais wa Uturuki, Tayyip Erdogan, alisema Jumatano kuwa mashambulizi ya Israel nchini Syria na Lebanon yamefikia kiwango ambacho sasa yanaihatarisha pia Uturuki. Aliongeza kuwa “uchokozi” wa Israel ni tishio kwa dunia nzima na lazima ukomeshwe.

Akilihutubia Bunge la Taifa, Erdogan aliishutumu Israel kwa kuchukua hatua ambazo zinaweza kuongeza ukosefu wa utulivu katika eneo la Mashariki ya Mediterania na kanda nzima.

“Usalama wa Uturuki hauanzi Hatay pekee, bali pia Aleppo, Damascus na Beirut. Hatuwezi kukubali hali yoyote ya kutumia nguvu katika nchi za ndugu zetu, wala hatutafumbia macho uchokozi,” alisema, akisisitiza kuwa usalama wa nchi yake unaenea zaidi ya mipaka yake.

Rais Erdogan pia aliashiria kile alichokiita “dhana potofu ya Ardhi ya Ahadi” ya Waisraeli, akisema kuwa Uturuki inaelewa kikamilifu lengo lao la mwisho.

“Kwa mapenzi ya Mungu, hatutaruhusu jambo hilo kamwe,” alisema.

Akiyaonya mataifa dhidi ya kujiweka upande wa Israel, Erdogan alisema: “Hakuna anayepaswa kutafuta hatari au kujiingiza katika majaribio yasiyo na busara. Hakuna anayepaswa kufuata mkondo wa mtandao wa mauaji wa Kizayuni.”

‘Israel lazima izuiwe’

Kiongozi huyo wa Uturuki alionya kuwa kushindwa kuzuia hatua za Israel kunaweza kuwa na madhara makubwa kwa kanda na kwa jumuiya ya kimataifa kwa ujumla.

“Ikiwa uharamia wa Israel hautakomeshwa, dunia nzima pamoja na eneo hili itabeba matokeo yake,” alisema.

“Israeli lazima izuiwe. Hili ni jukumu la ubinadamu ... historia haipaswi kuruhusiwa kujirudia.”

Erdogan pia alionya kwamba Uturuki itajibu kwa nguvu hatua yoyote itakayolenga haki za raia wa Uturuki au za Kupro ya Kituruki katika eneo la Mashariki ya Mediterania.

“Ikiwa haki za Uturuki na za Waturuki wa Kupro katika Mashariki ya Mediterania zitaguswa au kulengwa, nataka ijulikane kwamba majibu yetu yatakuwa wazi kabisa na makali sana,” alisema Erdogan.

CHANZO:TRT World and Agencies