| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Ajali ya ndege yaua 14 nchini Sudan Kusini
Ndege hiyo, aina ya Cessna inadaiwa kuruka kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Juba, saa moja na robo asubuhi na kudondoka umbali wa kilomita 20, toka jiji la Juba, kulingana na taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Usalama wa Anga ya nchi hiyo.
Ajali ya ndege yaua 14 nchini Sudan Kusini
Ndege hiyo, aina ya Cessna inadaiwa kuruka kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Juba./Picha:Wengine

Watu wapatao 14, wamefariki dunia siku ya Jumatatu kufuatia ajali ya ndege ndogo karibu na mji mkuu wa Juba, Sudan Kusini.

Ndege hiyo, aina ya Cessna inadaiwa kuruka kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Juba majira ya saa moja na robo asubuhi na kudondoka umbali wa kilomita 20, toka jiji la Juba, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Usalama wa Anga ya nchi hiyo.

Taarifa za awali, zinaonesha kuwa ajali hiyo ilisababishwa na hali mbaya ya hewa iliyopelekea uoni hafifu kwa rubani wa ndege hiyo.

Waliopoteza maisha katika ajali hiyo ni raia 12 wa Sudan Kusini na Wakenya wawili.

"Miili ya waathirika iliungua vibaya,” alisema mmoja ya waokozi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa.

Januari mwaka jana, watu 20 walipoteza maisha katika ajali ya ndege iliyotokea kaskazini mwa nchi hiyo.

Mwaka 2021, watu watano walifariki dunia baada ya ndege iliyokuwa mafuta kwa ajili ya Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) kuanguka.

 

CHANZO:AFP